• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MADAKTARI Bingwa waweka kambi ya siku tano Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 29th, 2024

Timu ya madaktari Bingwa kutoka mikoa ya Ruvuma,Songwe na Mbeya wameanza kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali kwa wananchi wa mkoa wa Ruvuma.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr. Louis Chomboko amesema ,kambi ya Madaktari bingwa katika Mkoa wa Ruvuma itakuwa ya siku tano kuanzia  Aprili 29 hadi Mei 4 mwaka huu.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Songea (HOMSO)Dr.Majura Magafu amesema,uchunguzi na matibabu hayo yatahusisha magonjwa ya akina Mama,magonjwa ya ndani kama vile shinikizo la damu,kisukari na figo.

Dr. Majura ameyataja magonjwa mengine yatakayochunguzwa ni magonjwa ya watoto,mifupa,upasuaji,macho,kinywa,meno,upasuaji wa midomo sungura,masikio,pua,koo,afya ya akili,ngozi,moyo,mfumo wa chakula na saratani.

Amesema, Wizara ya Afya na TAMISEMI inaendelea kuboresha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi kwa kuwatumia madaktari waliopo katika Hospitali za rufaa za mikoa,kanda,taasisi na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Kwa mujibu wa Dr. Majura,lengo kuu la kuwatumia madaktari bingwa waliopo katika Hospitali na taasisi za serikali ni kufikisha matibabu ya kibingwa kwa wananchi wengi na kwa wakati ili zisaidie wanannchi kupata huduma bora na kwa gharama nafuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanal Ahmed Abbas Ahmed ameipongeza serikali kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika maeneo mbalimbali ikiwemo katika mkoa wa Ruvuma.

Amewataka Madaktari Bingwa,kutowasubiri wagonjwa hadi wafike Hospitali badala yake, wahakikishe wanajikita zaidi katika kutoa elimu inayohusiana na madhara,namna ya kujikinga na pia kuwafuata wananchi waliko jambo litakalowezesha kuwafikia watu wengi.

Amesema serikali itaendelea kuwekeza kwa kutoa fedha na kuajiri wataalam kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Rehema Madenge,ametoa wito kwa wananchi kutumia fursa za kambi hiyo kupata huduma za kibingwa kwa gharama nafuu na kupunguza usumbufu wa kufuata huduma mbali na maeneo yao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.