• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

Makarani wadanganyifu watafutiwa dawa

Imewekwa kuanzia tarehe: July 23rd, 2022

Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani nchini Asangye Bangu amesema wamedhamiria kutumia mizani ya kieletroniki katika vyama vyote vya Msingi vya Ushirika (AMCOS)ili kukabiliana na makarani wadanganyifu ambao wamekuwa kero kwa wakulima .

Bangu alikuwa anazungumza na wakulima wa Chama cha Msingi cha Ushirika Mandawa Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi ikiwa ni ziara yake ya kutembelea wakulima wanauza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani katika mikoa ya Ruvuma,Lindi,Mtwara na Pwani.

"Tutaweka mizani ya kijiditali katika vyama vyote vya msingi na Ushirika ambayo itasoma namba ambazo mpimaji na mkulima wataona kisha itatoa karatasi iliyochapwa kwenye mashine badala ya kuandikwa kwa mkono",alisisitiza Bangu.

Amesema vipimo hivyo vya kieletroniki ambavyo vitapimwa kwenye AMCOS pia vitaonekana kwenye ghala kuu na Ofisi za Bodi Makao makuu kwa sababu vitakuwa tayari kwenye Mfumo wa kieletroniki.

Amesema kuanza kutumika kwa Mfumo huo  kwenye AMCOS zote kutaondoa kwa asilimia zaidi ya 70 malalamiko kwa wakulima wanauza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mkurugenzi huyo wa Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa stakabadhi ghalani ameitaja hatua nyingine ambayo wanatarajia kuichukua ni kuratibu wasafirisha wa mazao ya wakulima kutoka kwenye maghala ya kwenye AMCOS na kupeleka kwenye maghala makuu ya vyama vya Ushirika.

Amesema watahakikisha magari yote yamesajiriwa na watachukua hatua kwa dereva au mmiliki wa gari ambaye atabainika kuhujumu mazao ya wakulima.

Amesema uchunguzi walioufanya wamebaini malalamiko mengi yanatokea kabla mzigo haujafika kwenye ghala kuu .

"Lengo letu tunataka kila mtu aogope mali ya mkulima aone kama amekutana na moto,sipo tayari kuona wakulima wanaendelea kulalamika na kuona kama vile Mfumo wa stakabadhi ghalani haufai wakati wakulima wengi wanaupenda ",alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassa Ngoma akizungumzia Mfumo wa stakabadhi ghalani amesema mfumo huo unawasaidia wakulima wengi isipokuwa changamoto zilizopo wakati wa utekelezaji wa Mfumo huo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi.

Amesema wakulima hawana tatizo na Mfumo isipokuwa kinachotakiwa ni maboresha ili kuleta tija zaidi.

Ameunga mkono matumizi ya mizani ya kieletroniki ambayo amesema itamaliza udanganyifu wa baadhi ya makarani ambao sio waaminifu ambao wamekuwa wanadaiwa kuwapunja wakulima.

Said Mohamed Kassim Mkulima wa kijiji cha Mandawa Wilaya ya Ruangwa amesema kuna changamoto kubwa kwenye upimaji mizani ya kuandikwa stakabadhi kwa mkono ambapo kumekuwa na tofauti ya uzito hali ambayo inaleta shida kwenye malipo.

Ameunga mkono wazo la kufunga  mizani za kieletroniki kwenye AMCOS ambapo amesema zitamaliza changamoto hiyo.

Zuhura Ally Juma Mkulima wa kijiji cha Mandawa amedai mizani inayotumika kupima mazao yao hawana imani nayo wanaomba kubadilishiwa kwa sababu imekuwa inatoa vipimo tofauti na kuleta manung'uniko makubwa kwa wakulima wa korosho.

Zao la korosho ambalo litajwa kuwa dhahabu ya kijani ni zao la kwanza la kimkakati linalochangia maendeleo ya uchumi kwa wananchi na serikali kwa ujumla.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Julai 23,2022


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.