• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MASOKO ya madini ya vito na dhahabu mkoani Ruvuma yalivyowakomboa wachimbaji wadogo na kuinua Pato la Taifa

Imewekwa kuanzia tarehe: January 23rd, 2020

WILAYA ya Tunduru iliyopo mkoani Ruvuma imebarikiwa na utajiri wa madini mbalimbali ya vito  vya thamani na dhahabu.

 Endapo  madini hayo yangesimamiwa tangu yalipoanza kuchimbwa mwaka 1995,wachimbaji wadogo na serikali ingepata mapato makubwa katika mrabaha na kodi zinazotokana na mauzo ya madini hayo.

kipindi cha nyuma kabla ya serikali ya awamu ya tano,sekta ya madini ilishindwa kuwanufaisha watanzania ambapo Rais Dkt.John Magufuli baada ya kuingia madarakani amefanya mabadiliko katika sekta ya madini ikiwemo kufanya marekebisho katika sheria ya madini hali ambayo imesababisha watanzania kuanza kunufaika katika sekta hiyo.

Moja ya vitu ambavyo Rais aliagiza ni kuanzishwa kwa masoko ya wazi ya  madini kila Mkoa ambapo katika Mkoa wa Ruvuma yameanzishwa masoko ya madini  mawili moja katika wilaya ya Tunduru na soko la Mkoa mjini Songea.

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Jumanne Mohamed Nkana anasema  soko la wazi la madini ya vito na dhahabu  la mjini Songea lilifunguliwa Mei 3,2019 na soko la Tunduru lilifunguliwa Mei 27,2019.

Anasema tangu kufanyika kwa ufunguzi  wa masoko hayo hadi kufikia Desemba 31, 2019,jumla ya gramu 206,712 za madini ya vito ziliuzwa sokoni zikiwa na thamani ya shilingi zaidi milioni 513.

Anautaja mrabaha uliolipwa kutokana na mauzo hayo ni zaidi ya milioni 32 na ada ya ukaguzi iliyolipwa serikalini ni milioni 5.4 na kodi ya huduma kwa Halmashauri husika  ni zaidi ya  milioni 1.5.

Kwa mujibu wa Mhandisi Nkana,madini ya dhahabu katika kipindi hicho zimeuzwa jumla ya gramu 24,415.96 zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.310 ziliweza kuuzwa katika soko la madini la Songea.

Anautaja mrabaha ambao ulilipwa serikalini kutokana na mauzo ya dhahabu ni zaidi ya shilingi milioni 138 na ada ya ukaguzi iliyolipwa  ni zaidi ya milioni 23 na kodi ya huduma iliyolipwa kwa Halmashauri husika ni zaidi ya milioni 6.9.

“Kwa ujumla  katika masoko yote mawili ya Tunduru na Songea  tangu kuanzishwa kwa masoko haya hadi kufikia Desemba 31,2019 madini  ya vito na dhahabu yaliyouzwa  yalikuwa  na uzito wa  gramu 231,128.2 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.824’’,anasema.

Mhandisi Nkana anautaja mrabaha wa jumla uliolipwa serikalini ambao umetokana na mauzo ya madini ya dhahabu na vito katika kipindi hicho kuwa ni zaidi ya shilingi milioni 171 na ada ya ukaguzi iliyolipwa serikalini ni zaidi ya milioni 28.5 na kodi ya huduma ya jumla iliyolipwa katika Halmashauri husika ni zaidi ya  milioni 8.4.

Hata hivyo Nkana anakiri kuwa tangu kuanzishwa kwa masoko ya wazi ya madini ya vito na dhahabu kuna mafanikio kwa sababu kabla ya soko kuanzishwa kulikuwa hakuna takwimu zozote za mauzo ya madini kwa sababu wafanyabiashara wengi walikuwa hawalipi mrabaha na kodi nyingine zinazotakiwa kulipwa kwa mujibu wa sheria na mikataba ya madini.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Januari 23,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.