• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MDAHALO wa kitaifa wa maadili Songea waweka maazimio nane kukabiliana na mmomonyoko wa maadili

Imewekwa kuanzia tarehe: September 14th, 2024

MDAHALO wa kitaifa  wa  maadili uliondaliwa na Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo kuelekea tamasha la tatu la utamaduni la kitaifa  mkoani Ruvuma umeweka maazimio nane kukabiliana na mmomonyoko wa maadili nchini.

Akzungumza kwenye majumuisho ya mhadalo huo kwenye ukumbi wa Chandamali mjini Songea,Afisa Utamaduni Mwandamizi wa Kitengo cha Urithi na Maadili ya Taifa wa Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo Tito Lulandala ameyataja maazimio hayo kuwa ni  wazazi kuwajibika  vema katika malezi ya Watoto wao na jamii iweke mkazo Zaidi  katika malezi na makuzi yenye maadili.

Maazimio mengine ya kukabiliana na mmomonyoko wa maadili ni  wanasiasa katika ngazi zote wahamasishe uwajibikaji wa familia na jamii yote kwa ujumla katika kurithisha maadili mema kwa Watoto na vijana, jamii kulinda maadili na kuhakikisha malezi na makuzi bora ili wasiige tamaduni za kigeni.

Afisa Utamaduni huyo ameyataja maazimio mengine kuwa ni  wazazi na walezi kuelimisha watoto kuhusu madhara ya matumizi yasiyokuwa sahihi ya Sayansi na teknolojia ikiwemo mitandao ya jamii,viongozi wa dini kuhakikisha wanaifundisha jamii maadili mema,wazazi kuwa mfano wa kushiriki kwenye matukio ya kijamii  ikiwemo mikutano ya wazazi  shuleni na  wazazi na walezi kuwa karibu na Watoto wao ili kujua changamoto zinazowakabili na kutengeneza mazingira rafiki kwa Watoto ili wataja changamoto zao.

Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mdahalo huo, alikuwa ni Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt.Damas Ndumbaro ambapo amewataja wazazi na walezi kuwa wanaoongoza kwa kusababisha mmomonyoko wa maadili.

“Taasisi za malezi  na  makuzi zimebomolewa,familia zimebomolewa,utamaduni umepotea,dini zimeasiwa,tumevunja misingi ya jamii,utamaduni ndiyo kiboko ya mmomonyoko  wa maadili,tunaona fahari kuiga mambo ya nje kuliko mambo yetu’’.alisema.

Katika hatua nyingine Ndumbaro amesema Mkoa wa Ruvuma umepewa heshima ya kufanya tamasha la tatu la utamaduni la kitaifa ambalo linafanyika kwa siku nne katika uwanja wa Majimaji  Songea kuanzia Septemba 20 hadi 23 mwaka huu.

Amewaomba wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kujitokeza kwenye tamasha hilo ambalo litafungwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan Septemba 30 mwaka huu.

Katika mjadala huo wananchi wamepata fursa ya kuchangia mambo mbalimbali yanayosababisha mmomonyoko wa madili ambapo Alhaj Hamis Abdalah All  amewataja baadhi ya wazazi na walezi kuwa wanasababisha mmomonyoko wa maadili kutokana na tabia wanazozionesha mbele ya Watoto wao hivyo kuwa mfano mbaya kwa familia.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi  mkoani Ruvuma Dkt.Primius Nkwera  amesema maadili mema na upendo vikitawala katika familia vinaweza kupunguza mmomonyoko wa maadili huku akisisitiza sheria ichukue mkondo wake kwa watu wote wanaovunja sheria na kusababisha maadili mabovu.

Kwa upande wake Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma Mohamed Ally  ameshauri kuimarisha malezi,makuzi na maadili ya Watoto ili kurejesha maadili mema katika jamii.

Naye Shehe  wa Mkoa wa Ruvuma Ramadhani Mwakilima ameutaja utamaduni na maadili kuwa vinajengwa na dini ambapo amesisitiza mizizi mikuu ya maadili mema ni wazazi na walezi.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mathias Tilia  amesisitiza ili kuwa na maadili mema mafundisho ya msingi ya malezi  kwa Watoto yaimarishwe.

Kwa ujumla jamii nzima  wakiwemo wazazi,walezi,viongozi wa dini,walimu,wanasiasa na wadau wote wanatakiwa kusimamia maadili mema ili kukabiliana na mmomonyoko wa maadili.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.