• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFAHAMU Mzee aliyemficha Baba wa Taifa kwa saa kumi kwenye kihenge Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 12th, 2023

Na Albano Midelo,Namtumbo

TAMASHA kubwa la kutangaza fursa mbalimbali zilizopo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma linatarajia kufanyika kwa siku mbili kuanzia Septemba 22 hadi 23 mwaka huu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe.

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya anazitaja baadhi ya fursa katika tamasha hilo ambalo limepewa jina la Namtumbo Kihenge ni kutangaza fursa za uwekezaji kwenye sekta ya utalii kwa kuwa wilaya hiyo pia imebarikiwa kuwa na vivutio vya utalii wa kiikolojia,kihistoria na kiutamaduni.

“Sisi Wilaya ya Namtumbo ni miongoni mwa Wilaya nchini ambazo zimebeba historia kubwa katika harakati za kupigania Uhuru wa Tanganyika ambao ulipatikana mwaka 1961’’,alisema.

Analitaja eneo la kitongoji cha Mikulumo kata ya Luegu wilayani Namtumbo kuwa lina historia iliyotukuta hapa nchini kwa kuwa ni eneo ambalo alijificha baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere wakati anatafutwa na askari wa wakoloni katika harakati za kudai Uhuru  kuanzia Novemba 24 hadi 25,1955.

Anasema ili kulinda urithi wa eneo hilo serikali imeboresha mnara wa kumbukumbu ya Mwl.Nyerere na kwamba kati ya walinzi   wanne waliomlinda Baba wa Taifa alipojificha katika eneo hilo mwaka 1955,walinzi watatu wamefariki lakini,mlinzi mmoja mzee Maulid Hassan mwenye umri wa miaka 90 bado yupo hai na anaishi jirani na mnara huo.

Akizungumza namna alivyomficha Baba wa Taifa na kumuokoa kutoka kwa askari wa wakoloni waliokuwa wanamsaka Baba wa Taifa mwaka 1955,Mzee Maulid anasema kipindi hicho akiwa kijana wa umri wa miaka 20 aliambiwa na baba yake mzee Hassan kumficha Nyerere ili asikamatwe na wakoloni .

Anasema wazungu walipofika walimuulizia baba yake na yeye akajibu yupo mjini kwenye mkutano na kwamba kwa siku tatu alikuwa hajarudi nyumbani.

Mzee Maulid Hassan anabainisha kuwa  baba wa Taifa alimficha kwenye vihenge  vya baba yake vya kuhifadhia chakula ambavyo vilikuwa nyuma ya nyumba yao.

“Nilimficha Nyerere hapa kwenye vihenge wakati huo msitu ulikuwa mnene sana,tangu asubuhi alishinda kutwa nzima kwenye vihenge,mama alimpikia ugali wa ulezi na nyama ya kuku aliupenda sana nilikula naye na kushinda naye kutwa nzima kwenye vihenge,niliamua kwa ujasiri lolote na liwe, kama wazungu wakigundua bora mimi waniue na wamuache Nyerere’’,alisisitiza Mzee Maulid

Hata hivyo alisema muda wote aliokaa na Nyerere alikuwa anazungumzia Tanganyika kupata Uhuru kutoka kwa wakoloni na kwamba katika kipindi hicho yeye ndiye alikuwa mtu wa karibu wa Baba wa Taifa hadi alipochukuliwa jioni na kuondoka akiwa salama kabisa.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kata ya  Luegu Ditha Kayombo amelitaja eneo hilo kuwa lina utajiri wa historia ya Tanganyika kwa kuwa hadi sasa mzee aliyemficha Baba wa Taifa akiwa wilayani Namtumbo katika harakati za kudai Uhuru mwaka 1955 mzee Hassan bado yupo hai na serikali imejenga mnara wa kumbukumbu katika eneo hilo.

Anatoa rai kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuboresha eneo hilo kwa kuongeza majengo na wananchi waliopo jirani na eneo hilo wasogezwe pembeni ili eneo hilo  libaki kuwa kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere.

Ameishauri Serikali kuhakikisha Mzee Maulid Hassan aliyemficha baba wa Taifa ili kumuokoa na askari wa kikoloni mwaka 1955 anapatiwa huduma za msingi kama vile  maji,umeme,huduma ya afya na kujengewa makazi ya kisasa.

Serikali wilayani Namtumbo imeamua kwa vitendo kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha tamasha la Namtumbo Kihenge lililosheheni fursa lukuki za uwekezaji na uchumi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.