• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa stakabadhi ghalani wawaingizia wakulima Ruvuma zaidi ya bilioni 28

Imewekwa kuanzia tarehe: April 14th, 2021

MFUMO wa stakabadhi mazao ghalani katika Mkoa wa Ruvuma umewawezesha wakulima kupata fedha zaidi ya shilingi bilioni 28.

Akizungumza wakati anafungua mkutano wa wadau wa mazao ya ufuta,soya na mbaazi kwenye ukumbi wa Songea Club,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  amesema kiasi hicho cha fedha kimepatikana  katika msimu wa masoko wa mwaka 2020/2021.

Ameyataja mazao yaliuzwa katika mfumo wa stakabadhi ghalani kupitia minada mbalimbali iliyofanyika katika wilaya za Songea,Tunduru na Namtumbo kuwa ni  ufuta,soya na mbaazi.

Kwa mujibu wa Mndeme,zao la ufuta kilo 12,234,737 zilizouzwa na kuwaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni 25,soya kilo 1,499,077 ziliuzwa na kuwaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni moja na zao la mbaazi kilo 4,260,77 ziliuzwa na kuwaingizia wakulima zaidi ya sh.bilioni 2.585.

“Mfumo wa stakabadhi mazao ghalani umeonesha mafanikio makubwa katika Mkoa wetu,hivyo leo tunafanya tathmini ya msimu wa masoko uliopita 2020/2021 na kuratibu maandalizi ya msimu wa masoko wa 2021/2022 ambapo ununuzi unatarajia kuanza Mei 2021’’,alisema Mndeme.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amesema  mfumo huo umeziwezesha Halmashauri kukusanya ushuru kwa lengo la kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo kupitia zao la ufuta pekee zilikusanywa zaidi ya sh.milioni 954 za ushuru kwenye Halmashauri.

Mafanikio mengine ya mfumo huo ameyataja kuwa ni kufufuliwa kwa vyama vingi vya ushirika,kuongeza ajira na kwamba mfumo umerahisisha ukusanyaji wa kodi kwa ajili ya mapato ya serikali kuu kupitia TRA.

Awali akitoa taarifa ya mazao ya ufuta,soya na mbaazi kwenye mkutano huo,Mrajisi Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoani Ruvuma Bumi Masuba ameutaja uendeshaji wa masoko ya mazao hayo,ulifanyika kupitia vyama vya msingi 98 mkoani Ruvuma na kuleta mafanikio makubwa.

Ameyataja maandalizi ya masoko katika mkoa wa Ruvuma msimu wa 20201/2022 kuwa yanaendelea kufanyika kwa mfumo wa stakabadhi za ghalani kupitia vyama vya ushirika.

“Makadirio ya uzalishaji wa mazao hayo katika msimu huu ni ufuta tani 15,437,soya tani 7,844 na mbaazi tani 2,889’’,alisema Masuba.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 13,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.