• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa stakabadhi za ghala ulivyowanufaisha wakulima wa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 23rd, 2025

Wadau zaidi ya 70 wa kilimo, biashara na ushirika wamekutana Songea katika mkutano maalum wa kupitia mafanikio na changamoto za mfumo wa Stakabadhi za Ghala unaotumika kuuza mazao ya wakulima mkoani Ruvuma. Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Heritage Cottage Msamala, ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mheshimiwa Peres Magiri, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Magiri amesisitiza kuwa mfumo wa Stakabadhi za Ghala umeleta mageuzi makubwa kwa wakulima wa mkoa huo kwa kuwawezesha kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kupata malipo kwa uwazi na kwa wakati, endapo utatekelezwa kwa kufuata sheria na miongozo ya kitaifa.

Takwimu zilizowasilishwa kwenye mkutano huo zinaonesha kuwa katika kipindi cha misimu sita mfululizo kuanzia mwaka 2019/2020 hadi 2024/2025, mfumo huo umewezesha mauzo ya jumla ya tani 122,913.3 za mazao mbalimbali. Mazao yaliyouzwa ni pamoja na ufuta tani 59,787.8 kwa wastani wa Sh. 2,745 kwa kilo, soya tani 16,383.5 kwa wastani wa Sh. 1,035 kwa kilo, na mbaazi tani 46,742 kwa Sh. 1,181 kwa kilo.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Magiri, mfumo huo unatekelezwa kupitia vyama vya msingi vya ushirika chini ya usimamizi wa vyama vikuu vya TAMCU LTD na SONAMCU LTD, ambavyo vimesifiwa kwa kusimamia kwa ufanisi ubora wa mazao na utekelezaji wa minada ya kielektroniki.

Aidha, alionya juu ya vitendo vya utoroshaji wa mazao kabla ya minada rasmi, akisisitiza kuwa vyama vya ushirika lazima viheshimu muda wa kuanza minada na kuhakikisha malipo kwa wakulima yanafanyika kwa wakati. “Wakulima wetu wasikate tamaa na mfumo huu, tunahitaji uwajibikaji na uadilifu kutoka kwa wote wanaohusika,” alieleza Magiri.

Alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka watunza maghala kuzingatia viwango bora vya utunzaji wa mazao kwa mujibu wa miongozo ya Bodi ya Usimamizi wa Maghala, huku akiipongeza TAMCU na SONAMCU kwa mchango wao katika ustawi wa kilimo na uchumi wa mkoa wa Ruvuma.

Mkutano huo umetajwa kuwa jukwaa muhimu la kuimarisha ushirikiano kati ya wakulima, vyama vya ushirika na wadau wa sekta ya kilimo, kuelekea kujenga mfumo imara na endelevu wa masoko ya mazao ya kilimo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.