• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 300 zajenga chanzo kipya cha maji Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: March 29th, 2023

SERIKALI kupitia wizara ya maji,imetoa shilingi milioni 322 kujenga chanzo kipya cha maji cha Mkele ili kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa mji wa Mbinga mkoani Ruvuma.

Kaimu meneja wa kitengo cha usambazaji maji wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Mbinga mjini (Mbiuwasa) James Kida alisema,chanzo hicho kina uwezo wa kuzalisha lita 50,000 kwa siku na ujenzi wake umekamilika.

Alisema,walilazimika kujenga chanzo hicho ili kufidia upungufu wa maji uliotokana na utekelezaji wa mradi mpya wa maji wa Lusaka unaohudumia takribani watu wapatao 12,000 kutoka kata tatu za Ruhuwiko,Betherehemu na Matarawe.

“wakati mradi wa maji Lusaka unajengwa kwa kutumia uzalishaji wa maji wa kwanza,baada ya kukamilika kulijitokeza upungufu mkubwa wa huduma ya maji, kwa hiyo chanzo hiki kimejengwa mahususi ili kufidia upungufu uliojitokeza kwenye mradi huo”alisema Kida.

Kida alitaja vyanzo vingine vinavyohudumia wananchi wa mji wa  Mbinga ni Ndengu kilichojengwa mwaka 1984 na vyanzo vinne vilivyopo kijiji cha Tukuzi kwenye mlima maarufu wa Lupembe ambavyo vimejengwa mwaka 2018.

Kwa mujibu wa Kida,chanzo hicho kimeanza kutoa huduma na sasa hali ya upatikanaji maji kwa wakazi wa mji wa Mbinga imeongezeka kutoka wastani masaa 8 hadi 15 na kutoa fursa kwa Mbiuwasa kuongeza wateja wapya bila kuathiri upatikanaji wa huduma kwa wananchi wa maeneo mengine.

Amewashukuru wananchi kuachia eneo hilo ili litumike kuongeza uzalishaji wa maji,hata hivyo amewataka kuacha kufanya shughuli za kibidamu ikiwemo kilimo ndani ya mita 60 na kuhakikisha wana tunza na kulinda chanzo hicho kwa manufaa ya wananchi wengi na viweze kuwa endelevu.

Baadhi ya wakazi wa Mji wa Mbinga,wameipongeza Mbiuwasa kubuni chanzo kipya cha maji ambacho kimesaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika mji huo.

Joseph Kumburu mkazi wa mtaa wa Lusaka alisema,kabla ya maboresho yaliyofanywa na Mbiuwasa upatikanaji wa maji katika maeneo yao haukuwa wa kuridhisha kama ilivyo katika maeneo mengine ya wilaya ya Mbinga.

Amewapongeza wataalam wa Mbiuwasa kwa kazi nzuri waliyofanya katika kutekeleza miradi mipya ya maji ambayo imewezesha kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika mitaa mingi ya mji wa Mbinga na hivyo kutoa nafasi kwa wananchi kujikita zaidi katika shughuli za uzalishaji mali.

Alisema, awali kabla ya kutekelezwa kwa mradi huo na maboresho mengine ya miundombinu ya maji yaliyofanywa na Serikali kupitia mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira(Mbiuwasa) upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ilikuwa changamoto kubwa.

Alisema,walitumia kati ya masaa 2 na 3 kupata maji kutoka kwenye visima vya asili na wengine kwenda kuchota kwenye mito ambayo maji yake hayakuwa safi na salama kwa matumizi ya binadamu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.