• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIRADI yote saba yapitishwa na Mwenge wa Uhuru Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 12th, 2024

MBIO za Mwenge  wa Uhuru 2024 zimeikubali miradi yote saba yenye thamani ya shilingi bilioni 4.4 iliyoipitia katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya mradi wa maji wa Ngumbo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 Godfrey Mnzava,Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Masoud Samila amesema mradi huo unagharimu  Zaidi ya shilingi bilioni 2.5  na utekelezaji wake umefikia asilimia 100.

“Mradi unawanufaisha wananchi 11,080  waliopo katika vijiji sita vilivyopo katika kata za Ngumbo na Liwundi na mradi umepunguza umbali mrefu wa wananchi kutafuta huduma ya maji’’,alisema.

Mradi mwingine ambao umezinduliwa na Mwenge wa Uhuru 2024 ni mradi wa ujenzi wa barabara ya lami katika Mji wa Mbambabay,mradi huo ambao umekamilika kwa asilimia 100 umegharimu shilingi milioni 500 kujenga lami nyepesi yenye urefu wa kilometa 0.88.

Meneja wa  TARURA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Thomas Kitusi amezitaja faida za mradi huo kuwa ni Pamoja na kupunguza gharama za matengenezo ya mara kwa mara,kupunguza athari za kimazingira kwenye maeneo yanayochukuliwa changarawe na kuongeza mtandao wa barabara za lami katika Wilaya ya Nyasa kutoka kilometa nne hadi 5.1.

Mwenge wa Uhuru pia umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Lovund inayojengwa katika Kata ya Kilosa Mbambabay ambapo hadi sasa mradi umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 703 na unatarajia kutumia Zaidi ya shilingi bilioni 1,2 hadi kukamilika.

Mratibu wa Mradi huo Denis Katumbi  ameitaja miundombinu iliyojengwa kuwa ni  vyumba nane vya madarasa,nyumba tatu  za walimu,nyumba ya Mkuu wa shule,jengo la utawala,maabara tatu,matundu ya vyoo 17,maktaba,bwalo la chakula,uzio kuzunguka eneo la shule,taki la maji la lita 5,000 na kichomea taka.

Mwenge wa Uhuru pia umetembelea mradi wa uhifadhi wa mistu wa asili wa Namswea wenye ukubwa wa keta 23,046, ambao umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 42.

Msitu wa Namswea unaunganisha kata nne  ambazo ni Linga,Lituhi,Mbaha na Ngumbo na utekelezaji wa uhifadhi wa msitu huo umezingatia sera ya mpango shirikishi wa usimamizi wa misitu ambapo vijiji 11 vimeungabishwa kupitia Kamati za Maliasili za vijiji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.