• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKATABA wa ujenzi wa kiwanda kikubwa cha sukari cha bilioni 500 wasainiwa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: January 24th, 2024

MKATABA wa ujenzi wa kiwanda kikubwa cha sukari  chenye thamani ya shilingi bilioni 500  ambacho kinajengwa katika Kijiji cha Magwamila Kata ya Lilai Muhukuru wilayani Songea mkoani Ruvuma umesainiwa kwenye ukumbi wa Mkuu wa Wilaya Songea Januari 23,2024.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile amesema mkataba huo ni makubaliano ya awali baina ya viongozi wa Kijiji cha Magwamila na wawakilishi wa Songea Sugar Limited  ambayo ni tawi la kiwanda cha Kagera Sugar ambao hivi sasa wamewekeza nchini Uganda  na  wameamua kuanzisha tawi la kiwanda hicho mkoani Ruvuma .

“Mkataba umeshuhudiwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Songea,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na wawakilishi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania Kanda ya Nyanda za Juu Kusini  chenye makao makuu yake jijini Mbeya’’.alisisitiza DC Ndile.

Ndile amewataka wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla kujiandaa kuupokea uwekezaji wa kiwanda kikubwa cha sukari katika Katika Kijiji cha Magwamila.

Amesisitiza kuwa  wawekezaji  hao wanatarajia kuweka zaidi ya bilioni 500 katika kiwanda hicho, ambapo kiwanda kitazalisha tani zaidi ya laki moja kwa mwaka.

 Ameongeza kuwa kiwanda hicho kitaweza kuzalisha umeme ambao utaweza kuuzwa kwenye grid ya Taifa, pia kitazalisha mafuta aina ya ethane ambapo amesema kuwepo kwa kiwanda hicho kitaleta manufaa makubwa katika  wilaya ya Songe ana Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Kwa upande wake  Mchumi Mwandamizi wa Bodi ya Sukari Tanzania Joshua Mhando ameishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji.

Naye Mwakilishi wa Mwekezaji wa kiwanda hicho, Kapil Dave ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuweka utaratibu mzuri wa uwekezaji ambapo ameahidi kufanya uzalishaji wenye tija na wenye kuleta maendeleo chanya.

Eneo la uwekezaji wa kiwanda cha sukari linatarajiwa kuwa na ukubwa wa hekta 30,000 kati ya hizo hekta 22,000 zitakuwa kwa ajili ya kilimo cha miwa na hekta 8,000  kwa ajili ya ufungaji wa mitambo ya kiwanda, barabara za ndani, maghala, makazi ya watumishi, ujenzi wa huduma za kijamii.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.