• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma kuzalisha korosho tani 28,000

Imewekwa kuanzia tarehe: October 18th, 2024

Mkoa wa Ruvuma unatarajia kuzalisha na kuuza zao la korosho tani 28,000 katika msimu wa mwaka 2024/2025.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed  wakati anazungumza kwenye uzinduzi wa masoko ya zao la korosho  katika msimu wa mwaka 2024/2025  kwenye mkutano wa wadau wa tasnia ya korosho Mkoa wa Ruvuma uliofanyika kwenye ukumbi wa Skyway mjini Tunduru.

‘’Leo Oktoba 17,2024 tunafungua  msimu  masoko wa zao la korosho katika Mkoa wa Ruvuma,ni matarajio yangu kila mdau atashiriki vema kufanikisha  msimu wa masoko ya zao la korosho’’,alisema.

Amesema katika msimu uliopita wa mwaka 2023/2024 Mkoa wa Ruvuma katika kutekeleza malengo ya kilimo cha zao la korosho ulizalisha jumla ya kilo milioni 26  sawa na asilimia 60.

Ili kuhakikisha zao la korosho linatoa mafanikio kwa mkulima,Mkuu wa Mkoa amekiagiza Chama Kikuu cha Ushirika Tunduru TAMCU kuhakikisha kinasimamia vizuri  mfumo wa malipo kwa mkulima na  kuhakikisha Halmashauri zinawasimamia maafisa ugani katika zoezi la ukusanyaji mazao.

Maagizo mengine ambayo ameyatoa Kanali Abbas ni Halmashauri na vyama vya ushirika kuhakikisha vinasajili wakulima kwa kuzingatia majina yao halisi,benki zinatumia majina kamili ya wakulima ili kufanya malipo                                                     sahihi na wakala wa vipimo kusimamia matumizi  ya vipimo sahihi.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amemshukuru Rais  Dkt,Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyoimarisha sekta ya kilimo mkoani Ruvuma  likiwemo zao la korosho.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania Francis Alfred akizungumza kwenye mkutano huo amesema msimu wa mauzo na masoko ya ,korosho  wa mwaka 2024/2025 ulifunguliwa rasmi Septemba Mosi 2024.

Amesema minada imeanza rasmi Oktoba 11 mwaka huu  mkoani Mtwara na kwamba mnada wa kwanza mkoani Ruvuma unatarajiwa kufanyika Oktoba 29 ambapo amebainisha kuwa Mkoa wa Ruvuma katika msimu huu unatarajia kukusanya na kuuza korosho kilo 28,000,000.

Amesema Chama Kikuu cha Ushirika kwa kushirikiana na Bodi ya Korosho imeandaa mafunzo ya udhibiti ubora wa korosho kwa wenyeviti,mameneja,makarani wa vyama vya msingi vya ushirika AMCOS,wajumbe wa Bodi wa chama kikuu na maafisa ushirika wilayani Tunduru ambapo jumla ya washiriki 176 watapata mafunzo. 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.