• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma ulivyodhamiria kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 5th, 2023

MKOA wa Ruvuma umejipanga kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa kavu(Parchment)kutoka tani 19,000 katika msimu 2022/2023 hadi kufikia tani 75,000 ifikapo  mwaka 2025.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas amesema hayo , wakati akifungua mkutano wa mwaka wa wadau wa zao la kahawa kanda ya Ruvuma kilichofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoriki Jimbo la Mbinga.

Alisema,wastani wa uzalishaji wa kahawa kavu katika mkoa huo ulishuka kutoka tani 23,000 katika msimu 2021/2022 hadi kufikia tani 19,000 katika msimu 2022/2023.

Kwa mujibu wake, katika mkoa wa Ruvuma Kahawa inazalishwa katika Halmashauri saba ikiongozwa na Halmashauri ya wilaya ya Mbinga na Nyasa huku Halmashauri ya wilaya Tunduru ikiwa ni mdau mkubwa katika mnyororo wa thamani wa zao hilo.

Kanal Laban amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ya kukifanya kilimo kuwa biashara.

Alisema,mkakati huo umewawezesha wakulima kuwa wafanyabiashara na juhudi hizo zimesaidia sana kuongeza usafirishaji wa mazao ya kilimo nje ya nchi na kukuza kipato cha Wananchi wa mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Laban,amewaomba wadau wote kushikamana katika kuwekeza katika uzalishaji wa zao la kahawa hasa ikizingatiwa kuwa,ni moja kati ya mazao saba ya kimkakati yaliyoanishwa na serikali.

Aidha alisema,umuhimu wa zao  la kahawa unatokana na mchango wake katika kipato cha mtu mmoja mmoja,Halmashauri na Taifa kwa ujumla na kutoa wito kwa wadau kuongeza uzalishaji na unywaji wa kahawa kwa afya ambao upo chini kwa wastani wa asilimia 10.

Kuhusu mkakati wa Kitaifa wa miaka mitano wa kuendeleza sekta ya Kahawa 2020-2025 Kanal Laban alisema,serikali ya mkoa inaendelea kutekeleza mkakati huo ikiwani utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi inayotaka uzalishaji wa kahawa kuongezeka hadi kufikia tani 300,000 ifikapo mwaka 2025.

Kanal Laban,amewaonya maafisa ushirika kuacha tabia ya kuwanyanyasa na kutoa vitisho kwa viongozi wa vyama vya msingi(Amcos) wanapohitaji kupata ufafanuzi wa miongozo  ikiwemo kupitisha nyaraka  wakiwataka kutoa rushwa, jambo linalorudisha nyuma juhudi za serikali kuimarisha sekta ya ushirika nchini.

Badala yake,watumie nafasi zao kuwasaidia wakulima kupitia vyama vya msingi(Amcos) na Vyama Vikuu kuwatumikia wananchi ili kuongeza tija katika uzalishaji wa zao la kahawa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uendeshaji na maendeleo ya zao la Kahawa Tanzania Kajiru Kissenge, amewapongeza wakulima wa mkoa wa Ruvuma kwa kuongoza katika uzalishaji wa zao la kahawa aina ya Arabika.

Alisema,bodi ya Kahawa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imejipanga kuongeza uzalishaji wa zao hilo kutoka tani elfu72 hadi kufikia  tani  elfu 80 na kuongeza soko la kahawa Ulimwenguni inayolimwa hapa nchini.

Mjumbe wa Bodi ya Kahawa Tanzania Gottan Haule alisema,Bodi ya Kahawa inatambua mchango mkubwa unaofanywa na wadau wa zao hilo katika mkoa wa Ruvuma ambao ndiyo kinara kwa kuzalisha kahawa aina ya Arabika hapa nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.