• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma wakusanya mapato ya ndani kwa asilimia 134

Imewekwa kuanzia tarehe: February 21st, 2024

Na Albano Midelo,Songea

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas  ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kufanikiwa kukusanya mapato ya ndani zaidi ya shilingi bilioni 29.5 sawa na asilimia  134 katika kipindi cha mwaka 2022/2023.

Kanali Thomas ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Amesema TRA katika kipindi hicho wamefanya kazi nzuri ya kukusanya mapato kwa kuwa wamevuka lengo la makusanyo ya zaidi ya shilingi bilioni 21 ambapo amesema Uchumi wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika.

“Mkoa unaendelea kuimarika kiuchumi kwa kuimarika kwa miundombinu,shughuli za uzalishaji mali,biashara na ukewekezaji shughuli za uchimbaji madini hasa makaa ya mawe,maboresho ya uwanja wa Ndege wa Songea na biashara na nchi jirani za Msumbiji na Malawi’’,alisistiza RC Thomas.

Ameyataja mazingira ya kujifunzia na kufundishia  wanafunzi yamekuwa bora zaidi ambapo Mkoa uliletewa fedha za kujenga shule mpya 12 za msingi kupitia BOOST kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7,7 pia serikali ilileta fedha zaidi ya shilingi bilioni tano kujenga sekondari mpya tisa kupitia program ya SEQUIP.

Kulingana na Mkuu wa Mkoa katika kipindi cha mwaka 2022/2023 serikali imetoa shilingi milioni 900 kukarabati hospitali kongwe ya Tunduru na zaidi ya shilingi bilioni tatu zimetolewa na serikali  kujenga hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya Songea.

Ameongeza kuwa serikali imetoa shilingi bilioni 9.3 kujenga vituo vya afya 14  na kwamba serikali imenunua mashine ya CT scan na digital xray kwa ajili ya hospitali ya Rufaa ya Mkoa na mashine ya Xray kwa ajili ya hospitali ua Halmashauri ya Madaba.

Akizungumzia sekta ya kilimo,Mkuu wa Mkoa amesema serikali imeingiza mbolea ya ruzuku mkoani Ruvuma jumla ya tani 90,000  ambapo hadi sasa mbolea tani 62,540 zimesambazwa kwa wakulima.

 Maazimio yaliyopitshwa katika kikao hicho cha RCC ni Pamoja na kila halmashauri kutumia mapato yake ya ndani kujenga shule ya bweni ya wavulana na wasichana na kufanya ufuatiliaji wa ujenzi wa chuo cha SUA tawi la Tunduru.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.