• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUTANO wa kuzindua Jukwaa la wadau wa usimamizi wa Rasilimali za Maji kuzindiliwa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: November 30th, 2020

KATIBU Tawala msaidizi Jeremiah Sendoro amezindua Mkutano Mkuu wa Jukwaa la wadau wa usimamizi na uendelezaji wa Rasilimali za Maji katika Dakio la sehemu ya juu ya mto Ruvuma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Chritina Mndeme.

Mkutano huo umefanyika  katika ukumbi wa chuo cha Veta Mjini Songea na kuhudhilia wadau mbalimbali  kutoka mikoa mitatu Lindi,Mtwara na Ruvuma.

Akizungumza katika Mkutano huo wa Jukwaa la wadau wa Maji Sendoro amesema ni fursa kwa wadau kujadili na kutoa maoni na mapendekezo ya namna ya kutunza vyanzo vya maji ili visihalibiwe.

Sendoro amesema kwa upande wa  Serikali ya Mkoa wa Ruvuma imejipanga, wananchi wanaoishi sehemu ya mradi huu  itahakikisha unatekelezwa,nakuunda  jumuiya ya watumia maji, sheria za vijiji na Halmashauri ambazo zitalinda watumia maji wote ili asiwepo mtu wa kukosa maji au kupata maji kidogo kulingana na Mahitaji isipokuwa wote wafuate sheria zilizowekwa.

“Tutatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri,watendaji wa Kata na Makatibu Tarafa na viongozi wote  kuhakikisha wanatekeleza maazimio haya     kwamba wananchi wa Ruvuma  wanapata  Maji na yasichafuliwe wala kupotea bila utaratibu, maji haya tumeyalithi kutoka vizazi vilivyopita nasi tuwalithishe vizazi vijavyo”.alisema Sendoro

Amesema usimamizi na utunzaji wa Rasilimali za Maji kwa mfumo wa mabonde  unasimamiwa na Sheria ya Maji na11 ya mwaka 2009 kusimamia,kupanga,kuendeleza na kutunza Rasilimali za Maji nchi imegawanyika  katika mabonde 9.

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Ruvuma na Pwani ya kusini  Sudi Mpemba amesema anao wajibu wa kusimamia rasilimali za  Maji katika mabonde na utaratibu waliouanzisha  wa kuzindua  Majukwaa ya Mabonde na  kusimamia Maji umeanza ngazi ya Taifa ni mwongozo wa sera ya mwaka 2002.

Amesema kutakuwa na mwongozo unaelekeza kusimamia Maji ngazi ya Taifa na na ngazi inayoifuata ni Madakio na ndiomana leo tumekutana na wadau kuzindua Jukwaa la  usimamizi wa rasilimali za maji sehemu ya dakio la Mto Ruvuma kwa watumiaji wa sehemu ya juu ndiko kwenye chanzo cha maji sehemu ya matogoro na wanatumia Wilaya ya Mbinga,Songea,Nyasa na Namtumbo

Hata hivyo amesema kupitia jukwaa hili nikuwafanya wadau waweze kuzungumza namna bora ya kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji bonde la Maji na kuangalia  changamoto pamoja na kutatua Migogoro .

“Tunatambua watumia maji wapo wa aina mbalimbali kutoka kwenye mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali mfano shamba la kahawa Avivu,watumiaji wanaozalisha umeme,pia kuna wadau wa Halmashauri ya  Mbinga, Nyasa na  tupo hapa kuunda vikundi kwaajili ya usimamizi na tayari umeainisha kwenye mpango wa  usimamizi  na umekamilika na unahitaji kutekelezwa”.amesema mpemba

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia Maji Bonde la Ndanda Andrew Mwanjela amesema Kwa Mkoa wa Mtwara wamejipanga lakini wanapata changamoto ya uelewa wa  wananchi ni mdogo kwamba chanzo cha maji ni nini? na kutoa visingizio vya Elimu wakati wataalamu wanatoa kila mara,amesisitiza kupitia Jukwaa hili maamuzi yatolewe ili kulinda vyanzo vya maji na kuepuka uhaba wa Maji.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma

Novemba 30,2020.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.