• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma aagiza vyanzo vya maji Songea kulindwa

Imewekwa kuanzia tarehe: October 30th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amekagua vyanzo vya maji  kwenye miradi ya maji Ndongosi na Liula wilayani Songea  na kuagiza vyanzo hivyo kulindwa ili viwe endelevu.

Brigedia Jenerali Ibuge amesikitishwa na uharibifu wa vyanzo hivyo unaoendelea kufanywa na wananchi kwa kulima mazao na shughuli nyingine za kibinadamu hali inayosababisha vyanzo hivyo kuwa katika hatari ya kutoweka.

“Naagiza kila kijiji kuitisha mkutano mkuu wa kijiji,kati ya ajenda zake kuu,iwe ni namna gani ya kukabiliana na tabia hii ya kuharibu vyanzo vya maji,nimeona miti inavyoangushwa kama haina mwenyewe’’,alisema RC Ibuge.

Hata hivyo alisema serikali inapenda watu wajipatie kipato kutokana na kilimo,ametahadharisha kuwa shughuli za kinadamu ndizo zinazoathiri  vyanzo vya maji.

Ametoa rai kwa watalaam wote wa maji wakiwemo RUWASA na Bonde la Maji la Ziwa Nyasa,waende vijijini ili kutoa elimu ya mazingira kwa wananchi na kuweka ramani kwenye eneo zima ambalo  lenye vyanzo vya maji ambapo ameagiza utekelezaji wa maagizo hayo ufanyike kabla ya Desemba Mosi mwaka huu.

“Tusiseme tuna changamoto ya tabianchi ni sisi wenyewe ndiyo tunaoharibu kwa kukamata miti,kulima hadi kwenye kingo za mito ,tunachoma moto misitu na kuvunja sheria mbalimbali za mazingira’’,alisema RC Ibuge.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji  wa miradi ya maji ya kijiji cha Ndongosi na  Liula kwa Mkuu wa Mkoa,Meneja RUWASA Wilaya ya Songea Mhandisi Mathias Charles alisema mradi wa maji Ndongosi ulisanifiwa kwa zaidi ya shilingi milioni 332.

Hata hivyo alisema kati ya fedha hizo zaidi ya shilingi milioni 23 ni fedha za maandalizi ya mradi,zaidi ya shilingi milioni 51 ni za usimamizi na zaidi ya shilingi milioni 256 ni fedha za ujenzi wa mradi wa maji.

Ameutaja mradi wa maji Ndongosi ulisanifiwa kuhudumia wakazi wapatao 3,175 wenye mahitaji ya maji lita 119,062.5 kwa siku na kwamba chanzo cha maji kutoka mto Mlaimonga  kina uwezo wa kuzalisha maji lita 902,016 kwa siku na kwamba mradi umefikia asilimia 98.

Kuhusu mradi wa maji wa kijiji cha Liula,Mhandisi huyo wa maji amesema mradi huo awali, ulisanifiwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni moja ambapo RUWASA  kwa kutumia watalaam wake wa ndani wamefanikiwa kumaliza shughuli zote kwa shilingi milioni 56 ambapo mradi umekamilika na unahudumia watu wapatao 4,320.

Hata hivyo amezitaja changamoto kuu zinazoikabili miradi hiyo ni  uharibifu wa vyanzo vya maji unaofanywa na wananchi kwa kuchoma moto hovyo,kulima kwenye vyanzo na kukata miti.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 30,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.