• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Namtumbo aendelea na ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi

Imewekwa kuanzia tarehe: September 9th, 2023

Wananchi wa Kijiji Cha Mhangazi wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma waliandamana pamoja na kuamua kutojihusisha na shughuli zote za majitoleo Kwa ajili ya maendeleo ya Kijiji chao kutokana na kitendo Cha mwananchi  wa Kijiji hicho kukamatwa kamatwa na kufunguliwa kesi za kuonewa.

Akiongea mbele ya mkuu wa wilaya ya Namtumbo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji hapo Lenatus Rufunda alisema anawashukuru wananchi wa Kijiji chake kuandamana mpaka ofisi ya mkuu wa wilaya baada ya kuona anavyoonewa kuhusu eneo lake ambalo alipewa na Kijiji Kwa kufuata utaratibu wa kisheria.

Akiongea Kwa masikitiko makubwa alimwambia mkuu wa wilaya hiyo kuwa amewahi kufungwa mara Tatu gereza la Songea  Kwa kuonewa na mara ya Tatu wananchi wa Kijiji chake waliamua kuandamana  pamoja na kususia shughuli za Maendeleo na ndipo aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo Dkt Kenneth Ningu kulifuatilia jambo Hilo na kutolewa gerezani.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mhangazi Alifa Mapunda alimwambia mkuu wa wilaya mpya kuwa vikao mbalimbali vimekaliwa kuhusu mgogoro wa mwananchi huyo kuonewa hata hivyo mlalamikaji alikuwa anamtengenezea kesi za jinai na kuacha mgogoro wa mashamba na kumfunga Kwa kuwa yeye ni askari mstaafu alisema mwenyekiti huyo.

Mapunda alidai baada ya wananchi wake kuona vitendo vya uonevu Kwa mwananchi mwenzao waliamua kuandamana mpaka Kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo Dkt Kenneth Ningu na kuwahaidi kulifanyia kazi na Kisha kumtoa gerezani .

Hata hivyo mwenyekiti huyo aliongeza kuwa askari huyo mstaafu anayefahamika Kwa jina la Oscar Wonanje mkazi wa Kijiji Cha Kitanda hataki kufuata utaratibu wa kupata maeneo badala yake anatumia nguvu na kuwatisha wananchi Kwa kutaka kuwaua Kwa kutumia silaha alisema mwenyekiti huyo.

Fidelis Gausi kaimu mtendaji wa Kijiji hicho alimwambia mkuu wa wilaya mpya kuwa eneo Hilo lilikuwa na msitu mkubwa lakini baada ya Kijiji kummilikisha Lenatus Lufunda akajitokeza huyo askari mstaafu na kumtaka Lenatus aache hiyo ardhi akidai kuwa eneo Hilo lilikuwa eneo waliokuwa wanaishi wazazi wao kabla ya kuanzisha Kwa operesheni ya vijijini mwaka 1974.

Fransis Mpalaza afisa ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alifafanua kuhusu mpaka kati ya Kijiji Cha kitanda na Mhangazi kuwa ni mto Mhangazi kadiri ya Ramani na ofisi ya mkurugenzi ilishafika katika vijiji hivyo na kutafsiri Ramani hizo lakini Kijiji Cha kitanda wanaonekana kutokubaliana na Hilo.


MPalaza alidai kuwa mgogoro huo umepelekwa Kwa kamishna wa ardhi pamoja na migogoro mingine sugu Ili aweze kuitafutia ufumbuzi na kuondoa kero Kwa wananchi hao.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Ngollo Malenya kupitia mkutano huo aliagiza eneo linalogombaniwa kati ya Lenatus Lufunda na Oscar Wonanje lisimame kufanyika kazi mpaka hapo ofisi yake itakapojiridhisha juu ya mgogoro huo.

Malenya alimwagiza mkuu wa jeshi la polisi wilaya ya Namtumbo kufuatilia Oscar Wonanje anayelalamikiwa  kutaka kuwaua wananchi kuwa ni askari mstaafu kutoka jeshi Gani Ili waweze kuchukua hatua !

Mkuu wa wilaya aliwaambia wananchi kuwa askari anatakiwa kuwa mlinzi wa amani hata kama amestaafu lakini anaonekana ni kero kubwa Kwa wananchi alisema Malenya.


 .

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.