• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Songea azindua madarasa shule ya mchepuo wa kiingereza

Imewekwa kuanzia tarehe: November 2nd, 2022

WAZAZI na walezi wanaoishi kata ya Kizuka Halmashauri ya wilaya Songea,wanatarajiwa kuondokana na adha ya kuwapeleka watoto wadogo  maeneo mengine kusoma,baada ya kuanzishwa kwa shule ya msingi Mkombozi (Mkombozi English Medium School).

Shule hiyo inatarajiwa kuanza kudahiri  wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza ambao watakuwa wanasoma kwa lugha ya kiingereza isipokuwa somo la Kiswahili ambalo litafundishwa kwa lugha ya Kiswahili.

Hayo yamesemwa na  Mwalimu wa taaluma wa shule ya Sekondari Mkombozi Hills Jackob Kauzeni,wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa vyumba sita vya madarasa vitakavyotumika kwa wanafunzi wa madarasa ya awali na msingi kwa Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema.

Alisema,madarasa ya shule ya msingi ni sehemu ya mradi wa shule ya Sekondari Mkombozi Hills ilianza kujengwa mwaka 2020 ambapo uongozi wa shule  hiyo uliona kuna sababu ya kuanzishwa kwa shule ya msingi ya Kiingereza (English Medium School).

Alitaja sababu zilizopelekea kuanzishwa kwa shule hiyo ni baada ya kukosekana kwa shule ya English Medium katika Halmashauri ya wilaya Songea,hivyo wazazi na walezi wengi kulazimika kupeleka watoto wao nje ya Halmashauri kwa ajili ya kufuata masomo.

Aidha alisema,lengo lingine  la kuanzishwa kwa shule hiyo ni kuandaa msingi mzuri wa wanafunzi wanaojiunga na sekondari kuendana na kanuni ya ufundishaji na ujifunzaji wa masomo mbalimbali yanayofundishwa  kwa lugha ya Kiingereza.

Aliongeza kuwa,hadi sasa majengo mawili yenye jumla ya vyumba vya madarasa sita na ofisi mbili  yanaendelea kujengwa  ambapo ujenzi  wake unatarajiwa utakamilika mwezi Disemba mwaka huu.

Alisema, katika  ujenzi wa mradi huo wa shule ya msingi fedha zilizopangwa kutumika ni zaidi ya Sh.milioni 95 na mara baada ya kukamilika wataanza kudahili wanafunzi wa madarasa ya awali na darasa la kwanza.

Shule ya Mkombozi iliyopo kijiji cha Kizuka,kata ya Kizuka Halmashauri ya wilaya Songea,inamilikiwa na mkazi wa kijiji  hicho Franco Nditi, aliyeamua kutumia sehemu ya fedha zake zinazotokana na kilimo cha mahindi kujenga na kuanzisha shule miaka sita iliyopita.

Mkuu wa wilaya ya Songea Pololet Mgema,amempongeza Nditi kwa kuamua kuwekeza fedha zake kujenga shule ambayo itasaidia jamii ya wakazi wa kata hiyo na wilaya ya Songea kupata sehemu sahihi ya kupeleka watoto wao kupata elimu bora.

Mgema,amewaomba wazazi na jamii kwa ujumla kumuunga mkono Nditi kwa kupeleka watoto wenye umri wa kuanza elimu ya awali,shule ya msingi na Sekondari  katika shule hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kufundisha kwa lugha ya Kiingereza.

Mkuu wa wilaya alisema, ili kuendana na dunia ya ushindani ambayo inahitaji ushindani mawasiliano ni vema  mtu akafahamu angalau lugha mbili za kimataifa ambazo zitamuwezesha kuwasiliana na mataifa mengine.

Pia alisema,mzazi au mlezi anatamani sana kuona mtoto anapata elimu bora,hivyo ameisifu shule hiyo namna ambavyo inatambua kuwaanda wanafunzi wake kwenye misingi bora ya elimu.

“Niwapongeze sana uongozi na walimu wa shule hii kwa namna mnavyojitahidi kutoa elimu ambayo imeambatana na misingi ya malezi yaliyobora”alisema Mgema.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.