• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Wilaya ya Tunduru aagiza kuanza mnada wa ufuta

Imewekwa kuanzia tarehe: May 21st, 2023

MKUU wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Julius Mtatiro,amewaagiza viongozi wa Chama kikuu cha Ushirika wilayani humo Tamcu Ltd,kuanza minada ya zao la ufuta ili kuwasaidia wakulima kupata soko la uhakika na bei nzuri.

Alisema,kuanza kwa minada kutazuia wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu kwenda kwa wakulima ili kununua zao hilo kwa mfumo usiokuwa rasmi wa kangomba unaowakandamiza na kuwanyonya  wakulima.

Mtatiro ametoa agizo hilo , wakati akizungumza na wenyeviti wa vyama vya ushirika vya msingi(Amcos)na viongozi wa Chama kikuu cha Ushirika(Tamcu)katika kikao kazi kabla ya kuanza

kwa msimu wa ununuzi wa mazao wilayani humo.

Alisema,kwa kuwa wakulima wengi wameshavuna ufuta mashambani hakuna sababu ya kuchelewa kufanyika kwa minada ili wakulima wapate fedha mapema ili ziweze kuwasaidia kufanya maandalizi ya msimu ujao.

Mkuu wa wilaya,amewasisitiza viongozi wa Amcos kuhakikisha wanaajiri makalani wenye sifa,waadilifu,wenye huruma na wakulima na wachapakazi ambao watakwenda kusimamia sekta ya ushirika.Amewataka wasimamizi wa vyama vya  msingi vya ushirika kuacha kufanya kazi kwa mazoea,bali kuhakikisha wanabuni vyanzo vipya vitakavyoongeza mapato ili vyama vyao viweze kujiendesha na kuimarika kiuchumi badala ya kutegemea ushuru na makato yanayotokana na mauzo ya mazao.

Mtatiro amewaonya maafisa ugani wilayani humo,kuacha mara moja tabia ya kuzurura mjini wakifanya sterehe na kuacha kwenda  vijijini kuwasaidia wakulima kwani kufanya hivyo ni kosa na wanapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Katika hatua nyingine Mtatiro amesema,kuanzia msimu wa kilimo 2023/2024 dawa za kupulizia korosho zitafikishwa moja kwa moja kwenye vyama vya msingi(AMCOS) ambavyo vitahusika kugawa viuatilifu kwa wanachama wao,badala ya utaratibu  uliotumika katika msimu 2022/2023 wa kupeleka kwa viongozi.

Alisema,utaratibu wa msimu uliopita haukuwa mzuri kwa sababu baadhi ya wakulima hawakupata viuatilifu kwani kuna viongozi waliuza kwa watu ambao siyo wanachama wala wakulima kutokana na tamaa ya kupata fedha.

Mtatiro,amewapongeza wakulima kutokana na jitihada kubwa wanazofanya mashambani licha ya changamoto nyingi wanazopitia,hata hivyo amewakumbusha kuanza maandalizi ya msimu mpya wa kilimo mapema kwa kupalilia mashamba ya korosho na hata kuongeza ukubwa wa mashamba yao.

Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika(Tamcu)Imani Kalembo alisema,wameshaanza maandalizi ya msimu mpya kwa kusambaza viroba katika vyama vyote vya msingi kwa ajili ya kukusanya ufuta kutoka kwa wakulima kwenda kwenye maghala.

Ametoa wito kwa viongozi wa Amcos,kuanza mara moja kazi ya kukusanya ufuta na kuhakikisha ufuta wote unaofikishwa kwenye maghala unakuwa safi na wenye ubora kabla ya kufanyika kwa mnada.

Alieleza kuwa,kwa msimu wa masoko 2022/2023  Chama Kikuu kiliendesha minada mitano ya zao la ufuta ambapo jumla ya kilo 2,548,815.00 wenye thamani ya Sh.bilioni 7,710,700.00 ziliuzwa

Kalembo alisema, uzalishaji wa zao la ufuta umeongezeka kutoka kilo 2,219,283 msimu wa 2021/2022 hadi kufikia kilo 2,548,815 msimu 2022/2023 ambapo ni ongezeko  la uzalishaji kwa asilimia 12.93.

Alisema kuwa,bei ya zao hilo kwa msimu 2022/2023 iliendelea kuimarika na bei ya wastani ilikuwa Sh.3,019 kwa kilo ikilinganishwa na msimu 2021/2022 ambayo ilikuwa Sh.2,298.96.

Alisema,wakulima wameendelea kufurahi mfumo wa stakabadhi  ghalani kwa kuwa na manufaa zaidi baada ya bei ya mazao yanayouzwa kwa mfumo huo kupanda ukilinganisha na misimu ya nyuma ambayo ufuta uliuzwa na kununuliwa kwa mfumo wa soko huria.

Kwa upande wake Mrajisi msaidizi wa vyama vya Ushirika mkoa wa Ruvuma Peja Muhoja alisema,mazao yote ya kimkakati ya ufuta,korosho,kahawa na zao maarufu la mbaazi yataendelea kuuzwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.