• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MVUA zasomba madaraja 19 Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 23rd, 2024

MADARAJA 19 na baadhi ya barabara za maungio zimesombwa na maji mkoani Ruvuma kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) mkoani Ruvuma Mhandisi Silivanus Ngonyani wakati anatoa taarifa ya hali ya barabara na madaraja ya Mkoa wa Ruvuma kwa Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Mtela Mwampamba katika daraja la Njoka Kata ya Kizuka Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Mhandisi Ngonyani amesema ili kurejesha mawasiliano ya madaraja na maungio ya barabara zinahitajika Zaidi ya shilingi bilioni 2.2.

Hata hivyo amezitaja juhudi zinazofanywa na TARURA ili kukabiliana na changamoto ya kusombwa madaraja na maungio ni Pamoja na kuwaelekeza wananchi kutumia njia mbadala na  kuomba bajeti ya dharura ili kurejesha miundombinu katika hali yake.

Ameyataja baadhi ya maeneo yanahitaji ujenzi wa madaraja mapya ili kuweza kuhimili wingi wa maji unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Miongoni mwa madaraja mapya yaliyojengwa na TARURA ni daraja la Mto Njoka lililopo katika Kata ya Kizuka Halmashauri ya Wilaya ya Songea  ambapo serikali imetoa Zaidi ya shilingi milioni 600 kutekeleza mradi huo ambao umekamilika kwa asilimia 100.

Akizungumzia daraja hilo Mhandisi Ngonyani amesema kukamilika kwa daraja hilo ni muendelezo wa kazi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita ya kuendeleza uboreshaji wa barabara na madaraja na kwamba ujenzi wa madaraja unaendelea katika wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.

“Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 katika bajeti ya miundombinu ya barabara Mkoa wa Ruvuma umeidhinishiwa Zaidi ya shilingi bilioni 22.5, hadi kufikia Machi 2024,TARURA Ruvuma imepokea Zaidi ya shilingi bilioni 8.3 ambayo ni sawa na asilimia 37 ya bajeti ya matengenezo ya barabara na fedha za maendeleo’’,alisema.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa daraja la Njoka,Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Mtela Mwampamba amesema Mkoa wa Ruvuma ni Mkoa wa kilimo ambao unapata mvua nyingi ambazo zinaathiri miundombinu ya barabara na madaraja.

Ameutaja Mto Njoka mwaka jana  ulikuwa haupitiki kutokana na kutokuwepo daraja la kudumu ambapo serikali kupitia TARURA  imetoa fedha za ujenzi wa daraja la kudumu linalounganisha vijiji vya  Muhukuru, Mipeta,kizuka,Magagura hadi Matomondo ambapo sasa barabara hiyo itakuwa inapitika kwa mwaka mzima baada ya kukamilisha daraja moja la Mgugusi ambalo linajengwa katika mwaka wa fedha 2024/2024

Kassim Mbunda Mkazi wa Kitongoji cha Mgugusi Kata ya Kizuka kwa niaba ya wananchi anamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za ujenzi wa daraja la Mto Njoka ambalo limewezesha wanafunzi wanaosoma katika shule ya Ulamboni kuvuka kwenye daraja hilo.

Amesema kwa muda mrefu wanafunzi wengi walikuwa hawaendi shule kwa mwaka mzima kutokana ukosefu wa daraja na kwamba wananchi walikuwa wanapata shida ya kusafirisha mazao kutoka kwenye mashamba yao baada ya mavuno.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.