• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: June 11th, 2024

Mwenge wa Uhuru 2024 umeikubali miradi yote yenye thamani ya Zaidi ya shilingi bilioni moja iliyoipitia katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Akizungumza kwenye makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kati ya Halmashauri ya wilaya ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga,Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mheshimiwa Kisare Makori amesema Mwenge huo katika Halmashauri hiyo umekimbizwa jumla ya kilometa 110.9 na kutembelea miradi sita yenye thamani ya shilingi bilioni 1.1.

Akitoa taarifa ya ufunguzi wa mradi wa kituo cha Afya Litumbandyosi kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri hiyo Joseph Rwiza amesema hadi sasa Zaidi ya shilingi milioni 824 zimetumika kujenga kituo hicho ambacho kinahudumia wakazi 11,506 wa Kata ya Litumbandyosi.

Ametaja lengo la kujenga kituo hicho ni kusogeza huduma za afya kwa wananchi ili kupunguza gharama za matibabu kwa wakazi wa Kata hiyo yenye vijiji vinne vya Mabuni,Luhagara,Kingoli na Litumbandyosi.

Mradi mwingine uliopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni shamba la miti ya mitiki lililopo katika Kijiji cha Mabuni lenye jumla ya miti 2,692 linalomilikiwa na Festo Mhagama.

Mwenge wa uhuru pia umetembelea chanzo cha chemchem ya Mto Askofu uliopo katika Kijiji cha Paradiso Kata ya Ruanda ambapo Chemchem hiyo ina uwezo wa kuzalisha maji wastani wa lita 16,000 kwa siku na ipo katika  hifadhi ya msitu wa Kijiji cha Paradiso chenye wakazi wapatao 2,766.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Godrey Mnzava ameridhia kuzindua mradi wa madarasa mawili katika shule ya sekondari Ruanda ambayo yamegharimu Zaidi ya shilingi milioni 48.

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga pia umekagua kikundi cha wanawake kinachoitwa Umoja wa Wanawake Mbalawala ambacho kinaendesha mradi wa utengenezaji na uuzaji wa nishati ya makaa ya mawe ya kupikia ambapo jumla ya shilingi milioni 130 zimetumika kutekeleza mradi huo

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.