• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAMTUMBO walivyoboresha bwawa lenye ramani ya Afrika na kuvutia wengi

Imewekwa kuanzia tarehe: November 13th, 2023

Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imeendelea kufungua milango ya utalii kwa kuboresha vivutio vya utalii vinavyopatikana katika wilaya hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya amevitaja miongoni mwa vivutio vya utalii vinavyoendelea kuboreshwa kuwa ni  bwawa la Chengena lililopo kilometa sita kutoka mjini Namtumbo.

Akizungumza kwenye hafla iliyofanyika kwenye bwawa hilo,Malenya amesema bwawa hilo lenye umbo la ramani ya Afrika limeboreshwa  na kuchorwa majina ya nchi mbalimbali za Afrika na bendera zake.

“Mtu yeyote anaweza  kuingia kwenye  bwawa hili kwa kuingia kwenye boti maalum na kufanya utalii wa ndani,akafika Chad,Algeria,South Afrika, Kenya, Somaria na nchi mbalimbali ambazo zipo  ndani ya Afrika’’,alisisitiza DC Malenya.

Amesema wilaya ya Namtumbo imedhamiria kufikisha ujumbe kwa watanzania kuwa hakuna haja ya Kwenda kwenye nchi hizo,wakati unaweza  kufika kwenye nchi hizo kupitia bwawa la Chengena Namtumbo.

Amesisitiza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo itaendelea kutenga fedha  kwa ajili ya kuboresha vivutio mbalimbali vya utalii ili kuvutia watalii wengi kutoka ndani ya Mkoa wa Ruvuma na nje ya Mkoa.

Hata hivyo amesema anawashukuru wadau mbalimbali waliotoa fedha za kuanza kuboresha bwawa la Chengena ambazo zimewezesha kununua mitumbwi kwa ajili ya kufanya utalii wa ndani kwenye bwawa hilo na kuchora ramani za nchi za Afrika.

Wananchi wilayani Namtumbo walijitokeza kwa wingi kwenye kivutio hicho  na kushiriki kwenye michezo mbalimbali ikiwemo kuvutana Kamba na soka  ambapo Kaimu Afisa Utamaduni wa Halmashauri ya Namtumbo Shaibu Majiwa amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa kuboresha kivutio cha bwawa la Chengena na kuhamasisha michezo.

Amesema bwawa hilo lilikuwepo tangu zamani,hata hivyo halikuonekana kama kivutio cha utalii ambapo hivi sasa watalii  wanapata fursa ya kufanya utalii kwenye bwawa hilo.

Majua ametoa rai kwa wananchi wa Namtumbo na Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wanafika kwenye bwawa hilo kufanya utalii wa ndani.

Naye Katibu wa CCM wilaya ya Namtumbo Ndugu Acheni Mwinsheshe Maulid amesema wilaya hiyo imeamua kumuunga mkono Rais kwa kuhamasisha utalii ambapo amesema wilaya hiyo ina vivutio mbalimbali vya utalii vikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na kivutio cha eneo  la Luegu ambako alijificha Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwl.Julius Nyerere katika harakati za kudai uhuru mwaka 1955.

Katika hatua nyingine Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo amefunga tamasha la MANTRA CUP lililoshirikisha timu nane kwenye mchezo wa soka.

Ligi hiyo iliyofanyika kwenye kivutio cha utalii Chengena ilianza  Oktoba 28 mwaka huu na fainali kufanyika Novemba 12,2023 ambapo mshindi wa kwanza timu ya Bamiani FC imepewa shilingi 700,000,kombe na mpira mmoja.

  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.