• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NAMTUMBO Women Forum kuwabadilisha wanawake kifkra na kimawazo

Imewekwa kuanzia tarehe: October 15th, 2023

Na Albano Midelo,Namtumbo

WANAWAKE wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mheshimiwa Ngollo Malenya  wamefanya Jukwaa la Mwanamke (Namtumbo Women Forum)  lenye lengo ya kumbadilisha mwanamke kifkra na  kiuchumi.

Jukwaa hilo limefanyika kwa siku mbili kwenye ukumbi wa Mtakatifu Agnes Chipole mjini Namtumbo ambapo mamia ya wanawake kutoka mkoani Ruvuma wamefundishwa mada mbalimbali za kuwajengea uwezo kiuchumi.

Akizungumza kwenye kilele cha jukwaa hilo ambalo pia lilihudhuriwa na baadhi ya wabunge kutoka mkoani Ruvuma,Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Ngollo Malenya  amelitaja lengo la Jukwaa hilo kuwa ni kumwezesha mwanamke kiuchumi,kifkra na kimawazo ili aweze kuibadilisha jamii inayomzunguka.

“Nilizundua Jukwaa la Wanawake wa Namtumbo Oktoba 13 ili kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan,kwenye Jukwaa hilo zilitolewa mada mbalimbali  za kumwezesha mwanamke kiuchumi’’,alisisitiza Malenya.

Hata hivyo amesema Jukwa hilo limedhamiria kubadilisha Maisha ya mwanamke kifkra na kimawazo ili aweze kujitambua na kupiga hatua   kwa kusonga mbele ambapo amesisitiza mwanamke kutambua nguvu aliyonayo ili kuweza kujikimu kiuchumi na kifkra hasa katika kipindi hiki cha uongozi wa Awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Malenya amemshukuru Rais Samia kwa kupeleka miradi mbalimbali katika wilaya ya Namtumbo ambayo amesema inakwenda kuboresha sekta mbalimbali zikiwemo za elimu, umeme, kilimo, afya,maji,miundombinu na maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum mkoani Ruvuma Mheshimiwa Jakline Msongozi akizungumza kwenye kilele cha Jukwaa hilo,amewaasa wanawake kuzingatia mafunzo ambayo wameyapata bure ambapo amesema  mafunzo hayo yanayoweza kubadilisha Maisha ya wanawake wa Mkoa wa Ruvuma.

Amesisitiza kuwa mafunzo ya kuwejenga wanawake kiuchumi yataleta tija katika kuendeleza familia na kukuza uchumi wa wanawake, amempongeza Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwainua wanawake wa Tanzania .

Naye Mbunge wa Viti Maalum wanawake mkoani Ruvuma Mheshimiwa Mariam Nyoka amesema hii ni mara ya kwanza mkoa wa Ruvuma kufanya tukio kubwa la Jukwaa la wanawake wa Namtumbo lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya.

Amesema Jukwa hilo limewaunganisha sio wanawake wa Namtumbo pekee,bali wanawake wa Mkoa wa Ruvuma ambapo pia amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo kutumia tamasha la Namtumbo Kihenge,kutangaza fursa mbalimbali zilizopo wilayani Namtumbo.

Nyoka ameshauri wilaya nyingine mkoani Ruvuma ,kuiga mfano wa Wilaya ya Namtumbo kwa kuhakikisha wanafanya majukwaa ya wanawake ili kuwaendeleza wanawake ambao ni shingo ya familia.

Mheshimiwa Vita Kawawa ni Mbunge wa Jimbo la Namtumbo akizungumza kwenye Jukwaa hilo ,amempongeza Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni nne kujenga sekondari ya wasichana ya Mkoa wa Ruvuma iliyojengwa wilayani Namtumbo.

Amesema sekondari hiyo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 1000 wanaonzia kidato cha kwanza hadi cha sita  imeanza kuchukua wanafunzi mwaka huu,inakwenda kuwa mkombozi wa Watoto wa kike.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Ruvuma Elizabeth Ngongi  amesema jukwaa hilo limewafungua macho wanawake  kutokana na mafunzo mbalimbali waliyopata yakiwemo mafunzo ya  fursa za kiuchumi,elimu ya biashara,Saikolojia,Falsafa na Theolojia.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.