• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yachangia milioni 100.9 vifaa vya afya na elimu Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: January 22nd, 2024


BENKI ya NMB imetoa shilingi milioni  100.9 ili kusaidia maendeleo katika sekta za afya na elimu mkoani Ruvuma.

Hayo yamesemwa na Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Faraja Ngingo kwenye hafla ya kukabidhi madawati kwa shule za msingi Manispaa ya Songea iliyofanyika katika shule shule ya msingi Kiburang’oma ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas.

Ngingo amebainisha kuwa kati ya fedha hizo zaidi ya shilingi milioni 24 zilitumika kwa ajili ya ununuzi wa vitanda na magodoro katika hospitali ya Halmashauri ya Madaba na  shilingi milioni tano  zilitumika kutengeneza madawati 50 katika shule ya sekondari Matetereka.

Kulingana na Meneja huyo, shilingi milioni 33.7 zilitolewa katika Wilaya ya Nyasa kwa ajili ya ununuzi wa mabati katika shule za Lundo,Chinula,Limbo,Ndingine,Chiwindi na Nangombo.

Ameongeza kuwa NMB pia imetoa shilingi milioni 22 katika wilaya ya Songea kwa ajili ya kutengenezea madawati 220 katika shule za msingi Legele,Kiburang’oma,Lipupuma,Londoni na Mkuzo.

Ngingo amesema NMB imenunua bati 150 zenye thamani ya  shilingi milioni 5.25 kwa ajili ya shule ya msingi Ntungwe wilayani Namtumbo na kwamba NMB imetoa shilingi milioni 10.2  kwa ajili ya vifaa vya hospitali ya wilaya ya Tunduru.

“Sisi kama wadau tunawajibu wa kuunga mkono juhudi hizi za maendeleo kwa kusaidia jamii,tulipopata maombi haya ya kuchangia maendeleo ya elimu ,tuliamua mara moja kuja kushirikiana nanyi ili kuwa chachu ya maendeleo’’,alisisitiza Meneja wa NMB.

Hata hivyo amesema kwa miaka kadhaa NMB imekuwa ikisaidia miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Ruvuma kwa kujikita zaidi katika miradi ya elimu kuchangia madawati na vifaa vya kuezekea na kwenye afya kuchangia vitanda,magodoro na vifaa vingine vya matibabu.

Kwa upande wake mgeni rasmi kwenye hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameipongeza NMB kwa msaada huo mkubwa kwa wananchi wa Ruvuma.

Amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amejenga miundombinu mingi ya elimu na afya hivyo wadau wengine kama NMB wanapojitokeza kuchangia vifaa kwenye miradi hiyo wanaunga mkono moja kwa moja juhudi za serikali za kuwaletea maendeleo wananchi.

Ametoa rai kwa wadau wengine mkoani Ruvuma kuiga mfano wa Benki ya NMB katika kuchangia maendeleo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea Mheshimiwa Kapenjama Ndile ameishukuru NMB kwa kupunguza changamoto ya madawati na meza katika shule za msingi na sekondari Manispaa ya Songea.

Amebainisha kuwa katika shule za msingi zilizopo Manispaa ya Songea kuna upungufu wa madawati 5,863  na katika shule za sekondari  za Manispaa ya Songea kuna upungufu wa meza 6,600.

Wanafunzi  wanaosoma katika shule ya msingi Kiburang’oma Mary Komba na John Haule kwa niaba ya wanafunzi wenzao wameishukuru Benki ya NMB kwa Msaada wa madawati 40 ambayo yamepunguza uhaba wa madawati.

Benki ya NMB imezifikia wilaya zote nchini ikiwa na matawi zaidi ya 230,wakala zaidi ya 20,000 na wateja zaidi ya milioni sita.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.