• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yawasha moto Peramiho;Bonanza lenye elimu ya fedha na michezo lavutia wengi

Imewekwa kuanzia tarehe: June 7th, 2025

Benki ya NMB Kanda ya Kusini imeandika historia katika kijiji cha Peramiho A wilayani Songea,mkoani Ruvuma baada ya kuandaa bonanza kabambe la NMB Kijiji Day lililokusanya mamia ya wakazi wa eneo hilo kwa michezo, burudani, na elimu ya kifedha.

 Tukio hilo limebeba dhamira kubwa ya kuwafikia Watanzania wa vijijini kwa kuwapelekea huduma za kifedha karibu na maisha yao ya kila siku, kwa lengo la kuwainua kiuchumi na kijamii.

Bonanza hilo lilipambwa na shamrashamra za michezo mbalimbali kama jogging, kuvuta kamba, mbio za magunia, kukimbiza kuku, na mechi za mpira wa miguu na mikono, huku burudani na vicheko vikishamiri kati ya wananchi na wafanyakazi wa benki hiyo.

 Katika hekaheka hizo, NMB iliwaelimisha wanakijiji kuhusu umuhimu wa kuhifadhi fedha katika benki na namna ya kuendesha vikundi vya kijamii kwa njia salama na endelevu.

Akizungumza na vyombo vya habari, Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kusini, Roman Degeleki, alisema bonanza hilo ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo kufikisha huduma zake kwa wananchi wa vijijini ambao mara nyingi hukosa fursa ya huduma rasmi za kifedha.

“Tunahakikisha kila Mtanzania, popote alipo, anapata huduma ya kifedha kwa urahisi, salama, na karibu kabisa na makazi yake,” alisema Degeleki.

Wananchi walioshiriki bonanza hilo hawakusita kueleza furaha yao na faida walizopata.

Florence Luoga, kijana mkazi wa Peramiho, alisema michezo hiyo imekuwa chachu ya mshikamano miongoni mwa vijana.

Naye Pludensia Tawete alieleza alivyoelimika kuhusu usalama wa fedha kwa vikundi kujiunga na mfumo rasmi wa benki, badala ya kutegemea mtu mmoja.

 Godfrey Lupembe aliweka wazi kuwa elimu hiyo imefungua macho ya wanakijiji kuhusu faida za akiba benki, ikiwemo kupata mikopo kwa maendeleo ya vikundi.
Kwa kuchanganya michezo, elimu ya fedha, na burudani, NMB imedhihirisha kuwa huduma za kifedha si suala la mijini pekee bali ni haki ya kila Mtanzania.

 Bonanza la NMB Kijiji Day limekuwa jukwaa la matumaini, mshikamano, na mabadiliko chanya kwa jamii ya Peramiho,Ni muhimu taasisi nyingine za kifedha kuiga mfano huu, ili kujenga taifa lenye usawa wa kiuchumi na maendeleo jumuishi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBOLEA ya ruzuku yaipandisha kahawa nyasa kwa kiwango cha juu

    June 07, 2025
  • NMB yawasha moto Peramiho;Bonanza lenye elimu ya fedha na michezo lavutia wengi

    June 07, 2025
  • MBINGA DC Mail kuleta mapinduzi ya Biashara na ajira wilayani Mbinga

    June 07, 2025
  • MAPUMZIKO mema ya Sikukuu

    June 07, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.