• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NMB yazindua kampeni ya umeBIMA Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: April 11th, 2024

BENKI ya NMB,imezindua kampeni maalum inayojulikana kwa jina la UmeBIMA yenye kuhamasisha Watanzania kukata Bima kwa ajili ya kulinda shughuli zao ikiwemo biashara pindi wanapopatwa na majanga mbalimbali ya moto,mafuriko na ajali zinazoweza kusababisha mtu kupata ulemavu wa kudumu.


Meneja wa NMB kanda ya Kusini Faraja Raphael amesema,Kampeni inakwenda na utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kukata Bima na itafika katika mikoa mingine ya kusini Lindi na Mtwara.

Amesisitiza kuwa,kampeni ya UmeBIMA inakwenda sambamba na kampeni kubwa ya Bima ya faraja inayalenga zaidi kutoa mafao ya pole kwa mwananchi anapopatwa na changamoto ya msiba au ulemavu.

Kwa mujibu wa Meneja huyo,gharama ya Bima ya Faraja mteja anajiunga kwa Sh.200 na anapata fao kuanzia Sh.milioni 1 hadi 6 na inafanyika katika mikoa yote ya Tanzania na kwamba NMB inashirikiana na kampuni kumi za Bima ikiwemo kampuni ya Reliance Insurance Co Ltd

Akizungumza na wafanyabiashara wa soko kuu la Songea Faraja amesema,NMB imekuja na Bima ya Machinga ambayo itaweza kuwasaidia pale wanapopata changamoto na Bima hiyo na inapatikana kwa Sh.10,000 kwa mfanyabiashara mwenye mtaji wa Sh.laki tano na mwenye mtaji wa Sh.milioni 10 ataipata kwa Sh. 60,000.


Ametoa rai kwa wafanya biashara kuwa na Bima hiyo kwa sababu wanaweza kupoteza mali za Sh.milioni 10 kwa kutokata Bima inayopatikana kwa gharama nafuu kutoka kwenye kampuni ya Bima hapa nchini.


Amesisitiza kuwa,Bima hizo zitawasaidia wafanya biashara kuwa na uhakika na shughuli zao kwa sababu hakuna atakayesimama na hawatalazimika kuingia gharama yoyote pale watakapohitaji kuendelea na shughuli zao baada kutokea majanga.


Amesema,NMB kwa kushirikiana na kampuni  inatoa Bima za magari na afya inayojulikana kwa jina la Afya Salama inayokatwa kwa Sh.laki mbili na itatumika kwa watu wanne Baba,Mama na watoto wawili na iwapo wataongezeka watu wengine muhusika ataongeza Sh.80,000 na watapata matibabu kwenye Hospitali zote hapa nchini bila kupata usumbufu.


Mwakilishi wa kampuni ya Bima ya Reliance Insurance Joel Mwakalebela amesema,kwa muda mrefu wanashirikiana na Benki ya NMB kutoa aina ya Bima mbalimbali ikiwemo Bima za magari,bima za moto na bima kwa watu Binafsi na wizi inapotokea mfanyabiashara kuibiwa mali zake.


Mwakalebela,amewataka wananchi wa mkoa wa Ruvuma kukata Bima ili kuwa na uhakika wa maisha na shughuli zao za kila siku kwani kampuni hiyo imekuja na suluhisho la changamoto zinazoweza kujitokeza.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.