• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NYASA yachangia mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu kwa asilimia 100

Imewekwa kuanzia tarehe: May 31st, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ameipongeza Halmashauri ya Nyasa kwa kuchangia kwa asilimia 100.02 mfuko wa wanawake,vijana na wenye ulemavu.

Mndeme ametoa pongezi hizo wakati anafungua kikao maalum cha Baraza la madiwani la Halmashauri hiyo cha kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Kassim Majaliwa mjini Mbambabay.

Amesema Halmashauri hiyo katika kipindi hicho imeweza kuchangia zaidi ya shilingi milioni 42 sawa na kiasi kilichopangwa kuchangiwa katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2018/2019.

“Katika makusanyo ya mapato ya ndani kwa mwaka 2018/2019, mlikisia kukusanya shilingi 1,309,108,000.00 na mlifanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 1,099,708,811.00 sawa na asilimia 84,hongereni sana’’,alisema Mndeme.

Mkuu wa Mkoa pia ameipongeza Halmashauri ya Nyasa kwa kufanikiwa kupata hati safi kulingana na ripoti ya CAG ya mwaka wa fedha ulioishia Juni 30,2019,ambapo amesisitiza kuwa hati safi ni matokeo ya utendaji kazi mzuri wenye mchikamano na ushirikiano baina ya watalaam na madiwani.

Ripoti ya CAG inaonesha kuwa Halmashauri ya Nyasa imefanikiwa kupata hati safi miaka minne mfululizo,kuanzia mwaka 2015/2016 hadi 2018/2019 ambapo Mndeme ametoa rai kuendelea kupatikana kwa hati safi hizo iwe chache kuongeza bidii zaidi katika kazi ili kuendelea kufanya vizuri zaidi.

Mkuu wa Mkoa amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa Jimson Mhagama kuwalipa mara moja madiwani stahili zao za mwezi Mei na Juni ili waweze kulipwa kabla ya muda wao kuisha.

Katika hatua nyingine Mndeme ameagiza kufufuliwa kwa mazao ya michikichi na kokoa katika wilaya ya Nyasa ambayo hali ya hewa inafaa kwa mazao hayo.

“Taarifa niliyonayo hadi sasa wilaya nzima inalima kokoa hekari 40 tu,haitoshi,hali ya hewa na udongo tulionao ni rafiki katika mazao hayo,nawaomba madiwani na watalaam nipate taarifa ni hekari ngapi zinafaa kwa kilimo cha michikichi ili tuweze kuandaa kwa ajili ya kuleta miche na kupanda msimu huu’’,alisisitiza Mndeme.

Mndeme amesema lengo ni kuhakikisha kuwa mazao hayo yanakuwa miongoni mwa mazao ya biashara  katika Wilaya ya Nyasa na kuwa chanzo cha mapato kwa mkulima na kuunganisha nguvu na mazao ya korosho na kahawa.

Akizungumza katika kikao hicho Diwani wa Kata ya Lupingo Casbert Ngwata amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kwa kusimamia utendaji kazi wa Halmashauri na kusababisha Halmashauri nyingi kupata hati safi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amelipongeza Baraza la madiwani la Nyasa kwa ushirikiano mkubwa walioutoa katika kipindi cha miaka mitano na kufanikisha utekelezaji wa  miradi mbalimbali ya maendeleo .

IMEANDIKWA NA ALBANO MIDELO

AFISA HABARI MKOA WA RUVUMA

MEI 30,2020

MBAMBABAY 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.