• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

NYASA yapokea miche 40,000 ya michikichi toka Kigoma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 8th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa imepokea Mbegu Elfu Arobaini (40,000) za Michikichi kutoka Taasisi ya Utafiti TARI iliyopo Kihinga Mkoani Kigoma, ili kuanzisha kitalu cha miche na kusambaza kwa Wakulima wa Wilayani hapa.

Lengo la Uanzishaji wa kitalu hiki ni kuboresha na utekelezaji wa kilimo cha Mazao ya kimkakati likiwemo zao la michikichi. Halmashauri inalenga kupanda Hekta 240 katika Kata kumi na moja (11) zilizopo mwambao wa Ziwa Nyasa, ili kukabiliana na uhaba wa mafuta na kuwaongezea kipato wananchi.

Akipokea mbegu hizo kwa niaba ya wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mh.Isabela O. Chilumba amesema “Mbegu hizo ni Ukombozi mkubwa kwa wakulima kwa kuwa mbegu hii ni ya kisasa na inachukua miaka mitatu kuanza kuvuna”. Awali kulikuwa na Mbegu ya kienyeji ambayo ilikuwa ikichukua miaka zaidi ya mitano na kuendelea mpaka  kufikia kuvuna.

Mh. Chilumba ameongeza kuwa kwa Ukanda wa mwambao wa Ziwa Nyasa kuna Kata 11 ambazo zina uwezo mkubwa wa kustawisha zao hili la biashara kwa kuwa awali walikuwa wakitegemea Uvuvi pekee, sasa zao hili limekuja kuwakomboa wakulima ili waongeze kipato na  kupata mafuta ya kupikia ya Mawese kutokana na zao hili la Mchikichi.

Aidha ametoa wito kwa wakazi wa Wilaya ya Nyasa kuchangamkia fursa ya Kilimo cha Michikichi ili wakuze kipato cha kaya na kutatua tatizo la mafuta ya kupikia Nchini.

Awali Akikabidhi mbegu hizo Mkurugenzi wa kituo cha Utafiti cha TARI Kihinga, Dkt Filson Kagimbo amesema amefika kukabidhi na kuotesha mbegu hizo kama wakulima wa Nyasa walivyoomba na Wilaya ya Nyasa ni moja kati ya Wilaya ambazo zina udongo na hali ya hewa inayofaa kuotesha  zao la Mchikichi, Ikiwa ni Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Mh. Kasim Majaliwa kwa kuitaka TARI kuzalisha na kusambaza Michikichi nchi nzima.

Ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Nyasa kuchangamkia fursa ya kilimo cha Michikichi kwa kuwa Mbegu hii ni ya kisasa na inazalisha mazao mara tano ya michikichi ya kienyeji ambapo kwa hekta inazalisha Tani 4 hadi 5 za Mafuta, ukilinganisha na miche ya kienyeji inayotoa Tani 1.6 ya Mafuta ya kwa hekta pia.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nyasa Bw Jimson Mhagama amesema atahakikisha anawasimamia wataalamu wa kilimo ili waweze kuwahamasisha wananchi wazalishe kwa wingi zao la Michikichi.

Baadhi ya Wananchi wa kikundi cha Nuru kutoka Nanungu kijiji cha Likwilu ambao wana Shamba Darasa la mfano kwa ajili ya kuwafundisha wakulima wa zao la Michikichi Wilaya ya Nyasa wameipongeza Serikali Wilayani Hapa kwa juhudi za kuwaletea mbegu hizo na kuwapa mahitaji wanayotaka na Kuboresha Zao la Michikichi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.