• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RAIS DKT SAMIA ashusha neema kwa wananchi wa Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: January 10th, 2023

RAIS SAMIA ATOA BILIONI 60 KUJENGA BARABARA YA LAMI MBINGA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan  ametoa zaidi ya shilingi bilioni 60 kujenga kilometa 35 za lami wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya ujenzi huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma,Mhandisi Ephatar Mlavi amesema mradi  huo unahusisha ujenzi wa barabara ya lami ya Kitai  hadi  Lituhi yenye urefu wa kilometa 82.

Hata hivyo amesema kiasi cha fedha kilichotolewa na serikali kinahusisha ujenzi wa barabara ya lami kwa kipande cha  kutoka Kijiji cha Amanimakoro hadi Kijiji cha  Ruanda,barabara yenye urefu wa kilometa 35.

Ameutaja mradi huo kuwa ulianza kutekelezwa Juni  15,2022 ambao  unatarajiwa kutekelezwa kwa miezi 18, hivyo kukamilika Desemba 2023 ambapo amemtaja Mkandarasi wa mradi huo kuwa ni kampuni ya China Railway Seventh Group.

Amesema mradi huo unahusisha ujenzi wa kilometa 35 za barabara kwa kiwango cha lami,ujenzi wa madaraja manne,ujenzi wa makalaveti makubwa saba na ujenzi wa makalavati madogo 58 na kwamba hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 24.

“Barabara hii ina umuhimu mkubwa katika usafirishaji wa makaa ya mawe kwa sababu eneo hili lina migodi mingi ya madini hayo hivyo barabara hii itasaidia usafirishaji wa makaa ya mawe Kwenda sehemu mbalimbali nchini ikiwemo bandari ya Mtwara’’,alisisitiza Mhandisi Mlavi.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi wa barabara hiyo,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,Kanali Laban Thomas amempongeza Mkandarasi kwa kufanya kazi ndani ya mkataba ambapo amesisitiza kazi hiyo ikamilike mapema ili wananchi waanze kunufaika nayo.

Ameitaja barabara ya Kitai-Lituhi kuwa ni miongoni mwa barabara kubwa mkoani Ruvuma yenye urefu wa kilometa 82 ambayo inategemewa na Mkoa katika kukuza uchumi na kwamba inaunganisha wilaya za Mbinga na Nyasa ,pia inaunganisha Mkoa wa Ruvuma na Njombe kupitia wilaya ya Ludewa.

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuchukua uamuzi wa kizalendo wa kutekeleza mradi huo unaoufungua Mkoa wa Ruvuma kupitia barabara ya Kitai-Lituhi.

meandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Januari 10,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.