• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC awafunda watumishi wa umma Halmashauri ya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 4th, 2022

MKUU WA MKOA AWAFUNDA WATUMISHI WA UMMA NAMTUMBO  

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewaagiza watumishi wa umma kuhakikisha siku zote wanafanya kazi  kwa kufuata sera, sheria, taratibu na miongozo ya kiutumishi ili kuwatumikia wananchi kwa ufanisi na tija.

Kanali Laban ametoa maagizo hayo wakati anazungumza na watumishi wa umma wa Halmashauri hiyo wakiwa na madiwani katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo mjini Namtumbo.

RC Laban amehimiza watumishi hao kufanyakazi kwa ushirikiano,kuacha majungu na kuishi kwa upendo baina ya watumishi wote.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Chiriku Chilumba kuhakikisha watumishi wanapata haki zao za msingi  za kiutumishi,yakiwemo madai na stahiki zao walipwe.

“Natoa wiki mbili kwa DED  kuleta taarifa ofisini kwangu ni watumishi wangapi wameshalipwa haki zao na wangapi hawajalipwa kwanini hawajalipwa’’,alisema Kanali Thomas.

Amesema serikali imetoa shilingi bilioni 11 ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Namtumbo hivyo amekemea tabia ya udokozi wa mali ya umma kwa baadhi ya watumishi badala yake wahakikishe wanasimamia ipasavyo miradi yote ya maendeleo.

“Tufanye kazi kwa uadilifu na weledi kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati,tuache wizi wa pesa za miradi,tuongeza kasi ya ukusanyaji mapato ya ndani na kubuni vyanzo vipya vya mapato ili Halmashauri iweze kujiendesha’’,alisisitiza.

Amesema Namtumbo ina mazao mengi kama ufuta,mbaazi,soya na mpunga hivyo amewaagiza watendaji wa Kata na vijiji wanaokusanya pesa kwa kutumia POS wasimamiwe ili kuhakikisha pesa zote zinaingia serikalini.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi hao Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Chiriku Chilumba ameahidi kutekeleza maagizo na kuwasimamia watumishi wa umma  ili watekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria na miongozo ya kiutumishi.

Namtumbo ni wilaya ya kwanza kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kujitambulisha rasmi kwa watumishi wa umma tangu alipoteuliwa na Rais hivi karibuni kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Apirili 4,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.