• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC IBUGE awaagiza watendaji wasisubiri migogoro ya ardhi iwakute ofisini

Imewekwa kuanzia tarehe: July 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amewaagiza maafisa wa ardhi kutatua migogoro ya ardhi kwa kuwatembelea wananchi katika maeneo yao badala ya kusubiri migogoro hiyo kuwakuta maofisini.

RC Ibuge ametoa maagizo hayo  wakati anazungumza katika kikao kazi cha watumishi wa sekta ya ardhi mkoani Ruvuma ambacho kimeshirikisha watendaji mbalimbali wakiwemo wakuu wa Wilaya,wakurugenzi wa Halmashauri,makatibu Tawala wa wilaya na watumishi wengine ngazi ya wilaya na Mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Maelekezo mengine ambayo ameyatoa RC Ibuge kwa maafisa ardhi ni kuhakikisha wanafanyakazi kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya kazi,kutojiuhusisha kuomba na kupokea rushwa na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu sheria mbalimbali za ardhi.

“Ikumbukwe kuwa baadhi ya migogoro ya ardhi hutokea kutokana na wananchi kutofahamu sheria za ardhi,kwa hiyo kinachohitajika hapa ni uelewa wa sheria ili wananchi kuzifahamu’’,alisisitiza Ibuge.

Brigedia Jenerali Ibuge pia ameagiza kuendelea na ukamilishaji wa kazi zote za urasimishaji wa makazi holela katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma na kwamba kipaumbele kiwa katika  Halmashauri ya Manispaa ya Songea ambapo zoezi hilo linafanyika kwa kasi ndogo ukilinganisha na wingi wa maeneo yaliyojengwa kiholela.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa  ametoa rai kwa wananchi ambao maeneo yao yamechukuliwa kwa ajili ya uwekezaji na yanahitaji fidia kuendelea kuwa watulivu wakati serikali inatafuta fedha kwa ajili ya fidia.Maeneo yanayohitaji fidia yaliyopo Manispaa ya Songea ni Bonde la Mto Ruhila,eneo la EPZA Kata ya Mwengemshindo na barabara ya  By Pass ya Mtwara Corridor.

Katika kikao kazi hicho RC Ibuge amewaagiza wanasheria wa Halmashauri zote kwa kushirikiana na maafisa Ardhi na TAKUKURU  kutoa elimu ya namna bora ya kufany usuluhisho wa migogoro ya ardhi kwa wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi ya Kata kwa sababu wameonekana kuwa sehemu ya kikwazo katika kutenda haki kwa wananchi.

Akizungumza kwenye kikao hicho,Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ameshauri ili kutatua changamoto za ardhi,bajeti ya kupima ardhi iongezwe ili eneo kubwa la ardhi lipimwe kuepusha migogoro ambayo inatokana na maeneo mengi kutopimwa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Julai 13,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.