• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME aagiza ushirika kustawishwa kwa manufaa ya wanachama na Taifa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 25th, 2020


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amewaagiza wadau  mbalimbali wa ushirika,kuhakikisha kuwa ushirika unastawi kwa manufaa ya wanachama na taifa kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Mndeme,ushirika unalindwa na sera na sheria ya ushirika na kwamba wanachama wenyewe ndiyo wasimamizi wa shughuli za kila siku za ushirika ambapo ameagiza katika Mkoa mzima pawe na mpango kabambe wa kusimamia,kuimarisha na kuendeleza ushirika.”Tusiwaruhusu wanaotaka kupindisha sheria ili waue mfumo wa ununuzi wa mazao ya ufuta,mbaazi na soya katika Mkoa wetu,tusiwaruhusu wezi na wabadhirifu kuwa viongozi wa vyama vya ushirika’’,anasisitiza Mkuu wa Mkoa.

Wakulima  mkoani Ruvuma wamenufaika na bei kwa utaratibu  wa mfumo wa stakabadhi ghalani  hali iliyowezesha kuuza mazao kwa bei nzuri na kupata faida. Mndeme anasema  kabla ya mfumo huo bei ya Ufuta ilikua shilingi 1,500, Soya Tshs.500 kwa kilo na Mbaazi ilikuwa shilingi kati ya shilingi 100 na 200 kwa kilo moja.Anasema  baada ya kuanza kuuza mazao hayo kwa mfumo wa stakabadhi ghalani Ufuta umepanda bei toka shilingi 1500 hadi 4,110 kwa kilo na kwamba Mauzo hayo yaliwawezesha wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kupata kiasi cha shilingi bilioni 24 kutokana na mauzo ya zao la ufuta pekee.

Kulingana na Mndeme. wakulima kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani katika zao la soya walifanikiwa kuuza kilo moja toka shilingi 500 hadi hadi kufikia shilingi 850 kwa kilo moja  na mbaazi toka shilingi 150  kwa kilo hadi  shilingi 850.

“Mfumo huu wa stakabadhi za ghalani umeleta tija kwa wananchi na hivyo kuongeza uzalishaji kutoka tani 8,000 hadi 10,000 za zao la ufuta na Kufufuliwa kwa vyama vya Ushirika vya kilimo na Masoko kwani kabla ya kuanza mfumo  huu vyama vilivyokuwa vinafanya kazi ni 67  na baada ya mfumo huu kuanzishwa vyama vinavyofanya kazi ni 204 ‘’,anasema Mndeme.

Hata hivyo Mndeme anabainisha zaidi kuwa  Halmashauri mkoani Ruvuma zimepata na zinaendelea kupata ushuru na kukuza mapato ya ndani ambapo takwimu za uzalishaji na mapato ya wakulima kwa sasa ni rahisi kupatikana na kuwa wazi tofauti na kabla ya utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani.

 Mfumo wa Stakabadhi ya mazao ghalani katika Mkoa wa Ruvuma unatekelezwa katika mazao sita ambayo ni korosho, Kahawa, Tumbaku, ufuta, mbaazi na Soya na kwamba umeweza kuingiza fedha kiasi cha shilingi  634,797,630,064 kutokana na mauzo hayo.

Mndeme anasema uzalishaji wa mazao yanayouzwa kupitia mfumo wa Stakabadhi ghalani umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka ambapo zao la korosho mwaka 2015 uzalishaji ulikuwa tani 11,329,800 zenye thamani ya shilingi 13,594,800,000 ukilinganisha na mwaka 2020 uzalishaji umeongezeka hadi kufikia tani 24,625,824 zenye thamani ya shilingi  65,376,990,905.

“Zao la Kahawa mwaka 2015 uzalishaji ulikuwa tani 17,518,500 zenye thamani ya shilingi 66,570,300,000 na kwa mwaka 2019/2020 uzalishaji ni Tani 15,675,100 zenye thamani ya shilingi 64,048,458.600’’,anasema.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa  zao la tumbaku kwa mwaka 2016/2017 uzalishaji ulikuwa tani 160,855 zenye thamani ya shilingi 542,323,900 na kwa mwaka 2018/2019 uzalishaji wa tumbaku ulikuwa ni tani 1,247,814.75 zenye thamani ya shilingi 4,101,640,347.

Mndeme amelitaja zao la Ufuta uzalishaji mwaka 2018//2019 ulikuwa tani 8,428,268 zenye thamani ya shilingi 24,882,415,441 na kwa mwaka 2019/2020 uzalishaji ulikuwa ni tani 10,909,667 zenye thamani ya shilingi 23,687,790,987 na kwamba Ununuzi wa zao hili bado unaendelea.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 24,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.