• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC MNDEME atoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020

Imewekwa kuanzia tarehe: July 18th, 2020
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ametoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Parokia ya Bombambili mjini Songea .
  • Uchumi na pato la mtu kwa mwaka; Uchumi wa Mkoa hutegemea Kilimo ambapo zaidi ya asilimia 87 ya wakazi wake hupata riziki yao kupitia Kilimo na kuchangia pato la Mkoa kwa asilimia 75. Pato la Mkoa wa Ruvuma (Regional/Gross Domestic Product - GDP) limeongezeka kutoka Tshs. 3,680,359,000,000.00 mwaka 2015 hadi Tshs. 5,317,073,000,000.00 mwaka 2019 sawa na ongezeko la asilimia 44.47. Aidha, pato la Taifa la mtu (Per Capital income) kwa mwaka 2015 lilikuwa Tshs. 2,505,569.00 na limeongezeka hadi Tshs. 3,288,256.00 mwaka 2019 ikiwa ni ongezeko la asilimia 31.23 haya ni mafanikio makubwa yaliyofanywa na Rais wetu.
  •  
  • UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO

Mkoa wa Ruvuma umeendelea kutekeleza kwa mafanikio Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya CCM ya mwaka 2015-2020 kwa kuhakikisha kuwa Serikali katika ngazi zake zote – Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaendelea na jitihada za kuzikabili changamoto mbalimbali ikiwemo kuondoa umasikini, kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kuendeleza mapambano dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali za umma, kudumisha amani, ulinzi na usalama wa maisha ya raia na mali zao. Katika kipindi cha taarifa hii, Mkoa umepiga hatua za kimaendeleo katika sekta za kilimo, mifugo, ushirika, uvuvi, madini, maliasili, miundombinu, mawasiliano na uchukuzi, nishati, afya, elimu na maji. Aidha, kumekuwa na mafanikio katika Sekta ya maendeleo ya jamii na utawala bora, kama inavyoonekana kwenye maelezo yafuatayo kwa kina katika sekta zote.

 SEKTA YA ELIMU

  • Maelekezo ya Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2015 katika sekta ya Elimu ni kuhakikisha elimu katika ngazi zote inakuwa na ubora unaostahili ili kuwezesha vijana na makundi mengine kumudu ushindani wa soko la ajira ambalo wigo wake umepanuka ndani na nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Msisitizo mkubwa wa Serikali ni kuendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014.
  •  
  • Hali ya utoaji wa Elimu, taaluma Na miundombinu ya shule katika Mkoa 
  • Katika kutekeleza maelekezo ya Ilani, Mkoa umefanya jitihada mbalimbali katika kuboresha sekta ya elimu kwenye ngazi zote.
  • UTEKELEZAJI WA ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI TANGU 2015-2020

Idadi ya Shule; Tangu mwaka 2015 hadi 2020 Mkoa umekuwa na ongezeko la idadi ya shule za msingi 103 kutoka  idadi ya shule 670 zilizokuwepo  mwaka 2015 hadi shule  773 mwaka 2020. Shule za sekondari zimeongezeka kutoka idadi ya shule 111 mwaka 2015 hadi shule 205 kufikia mwaka 2020 sawa na asilimia 54 ambalo ni ongezeko la shule 94.

Uandikishaji wa  wanafunzi umeongezeka na kuimarika ambapo kuna ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza kwa idadi ya wanafunzi  50021  hadi kufikia Juni 2020 ukilinganisha na idadi ya wanafunzi 47978  mwaka 2015 sawa na  ongezeko la asilmia 4.2 .

Itaendelea


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.