• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC Ruvuma aagiza watumishi wa umma wanaohujumu mapato ya serikali wachukuliwe hatua

Imewekwa kuanzia tarehe: September 21st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Thomas Laban amekemea matumizi mabaya ya fedha za umma kuagiza kuchukuliwa hatua kwa watumishi wanaohujumu mapato ya serikali.

Kanali Laban ametoa agizo hilo wakati anazungumza na watumishi wa umma wakiwemo madiwani wa Wilaya ya Mbinga katika ziara ya kikazi ya kujitambulisha rasmi kwa watumishi baada ya kuteuliwa na Rais kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Agosti mwaka huu.

“Sitakuwa na masihara na mtu yeyote anayecheza na makusanyo ya fedha za umma kupitia POS ,matumizi mabaya ya fedha za umma ikiwemo kufanya ziara za mafunzo nje ya Mkoa ambazo hazina tija ni matumizi mabaya ya fedha za umma,sitaruhusu vibali vya ziara hizo’’,alisisitiza Kanali Thomas.

Mkuu wa Mkoa pia ameagiza kushughulikia maslahi ya watumishi wa umma kwa wakati na kuimarisha mahusiano mazuri kati ya watumishi wa chini  na wakuu wa  ili kuongeza ari na utendaji kazi.

Ametoa rai kwa watumishi wa umma kujiandaa na kusitaafu ambapo amewataka watumishi hao kutambua kuwa siku wanayoajiriwa ndiyo siku ambayo wanatakiwa kuanza kujiandaa kustaafu.

RC Thomas amewaagiza maafisa Ugani kusimamia zoezi la kusajiri wakulima kwa ajili ya zoezi la mbolea ya ruzuku Pamoja na kusimamia kilimo cha Pamoja huku akisisitiza usafi wa mazingira na upandaji wa miti kufanywa na kila kaya ili kutunza mazingira.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaagiza madiwani kuhakikisha wanasimamia miradi yote inayotekelezwa katika Kata zao na kusisitiza kuwa sio sifa kuwa na miradi ambayo haikamiliki.

Awali akizungumza kwenye kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mheshimiwa Aziza Mangasongo amesema watumish 176 wamepandishwa vyeo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambapo serikali imelipa zaidi ya shilingi milioni 440 za malimbikizo ya mishahara kwa watumishi.

Amesema licha ya Halmashauri hiyo kuwa na watumishi 2015 ,bado inakabiliwa na upungfu mkubwa wa matumishi katika kada za elimu,afya na maendeleo ya jamii.

Amezitaja changamoto kubwa zinazowakabili watumishi katika wilaya hiyo kuwa ni mikopo umiza, madeni mengi kwa watumishi na baadhi ya watumishi wanaokaribia kustaafu kutapelewa hali ambayo inapunguza ari ya utendaji kazi kwa watumishi.

Akizungumzia utekelezaji wa kilimo cha Pamoja,Mheshimiwa Mangasongo amesema wilaya imeandaa hekari 2000 katika Kijiji cha Matiri na hekari 123 katika Kijiji cha Ruanda kwa ajili ya utekelezaji wa kilimo cha Pamoja.

Wilaya ya Mbinga  ni moja kati ya wilaya tano za Mkoa wa Ruvuma yenye vitongoji 780 na vijiji 117.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 21,2022

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.