• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA azindua usajili wa Wamachinga kwa njia ya vocha

Imewekwa kuanzia tarehe: January 30th, 2024

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amezindua usajili wa wamachinga kwa njia ya vocha katika eneo la soko la Majengo Manispaa ya Songea.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo uliowashirikisha viongozi na wanachama wote wa Shirikisho la Wamachinga Mkoani Ruvuma,Kanali Thomas  amesema uzinduzi  wa usajili wa Wamachinga ni mafanikio makubwa kwa Wamachinga yaliyopatikana katika serikali ya Awamu ya Sita.

“Kupitia usajili huu serikali itaweza kuwa na taarifa sahihi za wanachama wa  Shirikisho la Umoja wa Mchinga (SHIUMA)  kwa nchi nzima na kuwezesha kuweka mipango yake vizuri katika kusaidia kukuza sekta hii muhimu ya wajasirimali wadogo’’,alisisitiza.

Amesema kwa muda mrefu Wamachinga walikuwa wanafanya shughuli zao kwa usumbufu ambapo hivi sasa baada ya kutambuliwa,serikali imeweza kufanikisha kuanzisha umoja wa SHIUMA na kwamba hivi sasa kila Halmashauri ndani ya Mkoa wa Ruvuma kuna uongozi ambao unashirikina na Mamlaka za serikali kusikiliza na kutatua changamoto za Wamachinga.

Ametoa rai kwa Wamachinga kuhakikisha vitambulisho vilivyotolewa na serikali wanavitumia vizuri kwa ajili ya shughuli zao ambapo amesema vitambulisho hivyo pia vinaweza kuwasaidia katika maswala mbalimbali ya kuwatambua.

Amesisitiza kuwa Mjasirimali mdogo akisajiliwa kwa njia ya mtandao atatambulika rasmi na viongozi Pamoja na wadau hivyo kuweza kukuza sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya Uchumi na uwezeshaji wananchi.

Hata hivyo amesema zoezi la utoaji vitambulisho lilisimama kwa muda na sasa serikali inaandaa utaratibu mzuri zaidi  kwa kushiriakina na Wizara ya Maendeleo ya Jamii ili kuboresha vitambulisho vya Wamachinga.

Amesema Mkoa umetenga maeneo rasmi waliyopangiwa Wamachinga kufanya shughuli zao na kwamba serikali itaendelea kuboresha miundombonu na mazingira wezeshi ili kutoa huduma bora.

Kanali Thomas amesema serikali imewezesha kupatikana mikopo kwa riba nafuu kupitia benki ya NMB kwa ajili ya Wamachinga na kwamba matarajio ya serikali baada ya miaka kadhaa Wamachinga wawe wafanyabiashara wakubwa .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa SHIUMA Mkoa wa Ruvuma Salum Masamaki  ameipongeza serikali kwa kutatua kero mbalimbali zinazowakabili ikiwemo suala la kupata mikopo ambapo amesema hivi sasa Wamachinga kutoka Manispaa ya Songea wameanza kunufaika na mikopo kutoka benki ya NMB,

Amesema mikopo hiyo inawawezesha wajasirimali hao wadogo kukuza na kuendeleza biashara zao na kwamba baada ya kujisajiri wataweza kutambulika na Taasisi za fedha hivyo kupata mikopo na elimu mbalimbali za fedha.

Masamaki amesisitiza kuwa usajiri huo utawawezesha kupata kitambulisho cha Shirikisho la Umoja wa Wamachinga hivyo kuweza kupata huduma zote zinazotolewa na Shirikisho.

Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akiwa na Mwenyekiti wa SHIUMA Mkoa wa Ruvuma Salum Masamaki kwenye uzinduzi wa  usajili wa usajili wa Wamachinga kwa njia ya vocha eneo la Majengo Manispaa ya Songea


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.