• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA awaagiza wakuu wa Idara kuandaa majibu ya Hoja za CAG

Imewekwa kuanzia tarehe: March 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amewaagiza  wakuu wa Idara katika Halmashauri kushiriki ipasavyo katika kuandaa majibu ya hoja na utekelezaji wa mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Kanali Abbas ametoa maagizo hayo kwa nyakati tofauti wakati anazungumza katika kikao  cha kujadili utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 katika Halmashauri za Nyasa,Mbinga Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo hayo baada ya kutoridhishwa na utekelezaji  wa maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya LAAC kwenye Halmashauri hizo.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Kamati ya Bunge ya LAAC Agosti 2023 ilitoa maagizo manne ambapo hadi sasa hakuna agizo hata moja lililotekelezwa,katika Halmashauri ya Nyasa LAAC ilitoa maagizo kumi ambapo kati ya maagizo hayo hadi sasa ni maagizo mawili tu yametekelezwa na katika Halmashauri ya Mbinga Mji kati ya maagizo Matano yaliyotolewa hakuna agizo hata moja lililotekelezwa.

“Hali ya utekelezaji wa maagizo ya LAAC hairidhishi kabisa,katika Halmashauri za Mbinga Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga hakuna hata agizo moja ambalo limetekelezwa na kufungwa hadi sasa,kwanini maagizo hayo yote bado hayajafungwa?’’,alihoji RC Abbas.

Kanali Abbas pia ameelezea mwenendo wa  ushughulikiaji wa Hoja na mapendekezo  ya CAG katika Halmashauri hizo tatu bado hauridhishi ambapo amewaomba waheshimiwa madiwani kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha hoja zinajibiwa ipasavyo na kuhakikisha kuwa hoja hizo hazijirudii tena.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa ameiagiza Sekretarieti ya Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na Menejimenti ya Halmashauri kupitia majibu na vielelezo vyote kabla ya kuwasilisha kwa CAG kwa ajili ya uhakiki.

Mkuu wa Mkoa pia ameziagiza Halmashauri hizo kuchukua hatua mapema za kinidhamu kwa watumishi wanazozalisha hoja .

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Rehema Sefu Madenge akizungumza kwenye kikao hicho  amesema hoja zote zilizoagizwa na LAAC zimetokana na utekelezaji wa shughuli kwenye Halmashauri husika hivyo Halmashauri zinahusika moja kwa moja kujibu hoja hizo.

Amesisitiza kuwa hoja hizo zilizoibuliwa zina majibu hivyo amewaagiza watendaji hao kuhakikisha wanajibu hoja zote ili zifungwe na kuweka mkakati thabiti wa kuhakikisha hoja hizo hazijitokezi tena.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbinga Mheshimiwa Deusderius Haule ameamhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuwa atasimamia kikamilifu kuhakikisha wanatekeleza maagizo ya kujibu hoja za LAAC na kutekeleza mapendekezo ya CAG.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Rehemu Sefu ,Madenge akizungumza kwenye kikao cha mapitio ya  utekelezaji wa maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Hesabu za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Nyasa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.