• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC THOMAS azindua miongozo mitatu itakayoboresha elimu Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: September 10th, 2022

RC RUVUMA AZINDUA MIONGOZO MITATU YA ELIMU

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amezindua miongozo mitatu ya usimamizi na uendeshaji wa elimu.

Hafla ya uzinduzi huo imehudhuriwa na wadau wa elimu kutoka wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma na kufanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Songea Girls mjini Songea.

Akizungumza kabla ya kuzindua miongozo hiyo Kanali Thomas amewaagiza wasimamizi wa elimu kusimamia na kuondoa changamoto ya baadhi ya wanafunzi  kutomudu stadi za Kuandika, Kuhesabu na Kusoma (KKK).

“Mkaondoe udhaifu wa baadhi ya viongozi katika usimamizi na ufuatiliaji,kasimamieni na kuweka mikakati ya kupunguza au kuondoa kabisa uhaba wa miundombinu ya shule hasa vyoo vya wanafunzi’’,alisema RC Thomas.

Mkuu wa Mkoa amewaagiza wadau wote wa elimu kuondoa utoro wa baadhi ya wanafunzi na walimu.

Hata hivyo amesema miongozo hiyo imechambua changamoto mahususi katika  elimu ya awali,msingi na sekondari na kwamba mikakati ya muda mfupi na mrefu ya utatuzi wa changamoto imebainishwa katika miongozo hiyo.

Awali Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Jeremiah Sendoro aliitaja miongozo mitatu ambayo imezinduliwa kuwa ni  Mwongozo ambao umeainisha changamoto katika elimu ya msingi na sekondari.

Ameutaja mwongozo wa pili kuwa  unahusu mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji katika ngazi ya elimu ya msingi na mwongozo wa tatu umeeleza kuhusu uteuzi wa  viongozi wa elimu katika mamlaka za serikali za  mitaa na mikoa.

Hata hivyo amesema miongozo yote mitatu imebeba changamoto na taratibu za usimamizi na uendeshaji wa elimu ya msingi na sekondari na kwamba miongozo hiyo inakusudia kuleta tija katika sekta ya elimu kwa kutumia rasilimali zilizopo.

Naye Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma Emanuel Kisongo amesema miongozo hiyo inatarajia kuwa ni muarubaini wa changamoto za elimu hapa nchini.

Kisongo amesisitiza kuwa  miongozo hiyo imebeba zana ya kurudi darasani na kuwapa wanafunzi kile kinachostahili na kwamba wadau wote wa elimu wanatakiwa kusimamia kikamilifu utoaji elimu.

Miongozo hiyo mitatu imeundwa Julai mwaka huu kupitia Wizara ya TAMISEMI ikiwa ni juhudi za serikali ya awamu ya sita kuboresha elimu ili wananchi wake wapate elimu bora na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Tanzania.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 10,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.