• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

REDCROSS Mkoa wa Ruvuma ilivyofanikiwa kuhamasisha uchangiaji damu chupa 800

Imewekwa kuanzia tarehe: June 15th, 2020

REDCROSS Ruvuma ilivyohamasisha uchangiaji damu chupa 800

MRATIBU wa Damu Salama katika Mkoa wa Ruvuma Imani Mbuzi amelipongeza Shirika la Msalaba Mwekundu(Red cross) Tanzania Mkoa wa Ruvuma kwa kuhamasisha uchangiaji damu chupa 800.

Mbuzi ametoa pongezi hizo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma ambayo siku ya kilele cha maadhimisho ya uchangiaji wa damu kitaifa ambayo yalianza Juni tano hadi Juni 14 mwaka huu.

“Shabaha ilikuwa ni kila Halmashauri kuchangia chupa 100 za damu na kufanya jumla ya chupa 800 katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma,kutokana na uhamasishaji mkubwa unaofanywa na Redcross  tutavuka lengo kwa sababu idadi ya watu wanaojitokeza ni kubwa’’,alisisitiza Mbuzi.

Amesema katika kituo cha hospitali ya Rufaa ya Mkoa hadi sasa zimekusanywa uniti zaidi ya 55 na kwamba idadi ya watu wanaojitokeza kuchangia damu imeongezeka kutoka watu wawili kwa siku  hadi 12 kwa siku  na kwamba hali hiyo imetokana na uhamasishaji mkubwa unaofanywa na Redcross Mkoa wa Ruvuma.

Amesema Redcross wamefanyakazi kubwa ya kwenda kwenye mikusanyiko ya watu  kama sokoni,nyumba za ibada, madereva wa pikipiki,barabarani na kuhamasisha kuchangia damu hali ambayo imesababisha wengi kujitokeza.

Amesema bila Redcross uchangiaji wa damu mwaka huu ungekuwa na changamoto kubwa kutokana na janga la corona ambalo limesababisha kushindwa kuweka mahema sehemu za wazi  na kutangaza ili watu wafike kuchangia.

Mwenyekiti wa Redcross Mkoa wa Ruvuma Judith Kapinga amesema wateja wote ambao wamehamasishwa katika maeneo mbalimbali hivi sasa wanafika kwenye vituo vya kuchangia damu.

Amesema mwitikio wa watu ni mkubwa licha ya kukabiliwa na changamoto za kuacha shughuli zao kwa muda na kufika kuchangia damu vituoni na kwamba Redcross imedhamiria kuvuka malengo ya uchangiaji damu ili kuwa na benki ya kutosha ya damu na kuokoa maisha ya watanzania wanaohitaji damu.

“Wahitaji wa damu ni wengi wakiwemo mama wajawazito,watoto  chini ya miaka mitano,watu waliopata ajali,watu waliozaliwa na seli nundu na watu wanaofanyiwa upasuaji,hawa wote ni wahanga wa damu’’,alisisitiza.

Deredia Hamuya ni Mhamasishaji wa uchangiaji wa damu kutoka Redcross Mkoa wa Ruvuma,amesema Redcross imeshiriki kikamilifu kuhamasisha katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma ili  wajitokeze watu wengi kuchangia  damu na kuokoa maisha.

“Baada ya kuhamasishwa wengi wamejitokeza,wameelewa nini maana ya uchangiaji damu,suala la uchangiaji damu ni la kila mtanzania,thamani ya damu hailinganishwi na kitu chochote changia damu okoa maisha’’,alisema.

Zoezi la uhamasishaji wa uchangiaji damu linafanyika nchini kote kila baada ya miezi mitatu ambapo linatarajiwa kufanyika tena Septemba mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Juni 14,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.