• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RPC RUVUMA awaasa madereva kufuata sheria na kanuni za barabarani

Imewekwa kuanzia tarehe: March 25th, 2022

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Ruvuma Joseph Konyo amewataka madereva wote kufuata sheria na kanuni za barabarani ili kuepuka  ajali zisizo za lazima.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Songea Club Manispaa ya Songea.

Akizungumza katika kikao  hicho Kamanda Konyo amesema kuna changamoto chache ambazo zinaleta mtazamo hasi kati ya jeshi la Polisi na madereva hivyo amesisitiza wafuate sheria na taratibu zote kama kuvaa kofia ngumu, kuwa na leseni, kuendesha mwendo mzuri na kupaki sehemu sahihi ili kuepuka migogoro na Jeshi la Polisi.

‘’Naungana mkono wa dhati kabisa na waliosema kazi ya bodaboda na bajaji ni kazi sawa na kazi nyingine, na kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda raia na mali zao na madereva wa bajaji na bodaboda  wana mali zao lazima tuwalinde’’, amesema RPC Konyo.

Aidha, RPC Konyo amesema mwaka 2020 kuanzia Januari hadi Desemba ajali za pikipiki zilikuwa 16 watu waliofariki kwenye ajali hizo walikuwa 22 majeruhi 13 na pikipiki zilizoathirika na ajali zilikuwa 26, na kwamba kwa mwaka 2021 ajali zilikuwa saba, watu waliokufa wanne, majeruhi sita  na pikipiki 12 zilizoathirika na ajali hiyo.

RPC konyo ametoa rai kwa madereva wote kwa ujumla kujitokeza kushiriki Sensa ya Watu na Makazi ambayo inatarajia kufanyika Agosti 2022.

Kwa upande wake Kamnada wa Usalama Barabarani Mkoa wa Ruvuma RTO Salum Morimori amelitaja tatizo kubwa ambalo lipo kwa madereva wa bodaboda na bajaji ni kutokuwa na utayari wa kuhudhuria mafunzo ya udereva na kupata leseni, hivyo amewashauri madereva hao kutumia Elimu waliyoipata darasani na kufuata sheria zote za barabarani ili kupunguza ajali.

Naye Katibu wa Umoja wa Madereva Bajaji Songea Albert Nchimbi ameomba madereva waelekezwe , waonywe na wapewe Elimu juu ya makosa wanayoyafanya kabla ya kuandikiwa faini na kuwekwa mahabusu.

Imeandikwa na Bahati Nyoni

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Machi 24 2022.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.