• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA ilivyojipanga kwa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024

Imewekwa kuanzia tarehe: October 7th, 2024

Na Elizabeth Newa - Rs Ruvuma

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 11 mwaka huu kila mmoja ana wajibu wa kufanya kuhakikisha maandalizi yanakamilika kabla ya siku ya uchaguzi.

Kanali Ahmed ameyasema hayo wakati akizungumza na wadau wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

"Tukio ama shughuli mojawapo ni utoaji wa elimu au kuwapasha habari wananchi kuhusiana na zoezi hili na wajibu wao, hata kikao hiki ni sehemu muhimu ya maandalizi ya uchaguzi huu," alisema Kanali Ahmed.

Ameongeza kuwa tukio lingine ambalo litafanyika kabla ya uchaguzi ni uandikishaji wa wapiga kura ambao utaanza tarehe 11-20 Oktoba, 2024 hivyo amezitaka Wilaya zote na Halmashauri kuwahamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha.

"Sisi kama wadau ni muhimu tushirikiane kuhakikisha eneo hili linafanikiwa, kama tukifanya vizuri katika maeneo haya matukio mengine ya kampeni na siku ya kupiga kura yatafanyika vizuri,"alisema.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bi. Mary Makondo amesema wote kama wadau wanapaswa kushirikiana kuwahimiza wananchi wajitokeze kujiandikisha ili wapate sifa za kupiga kura.

Kwa upande wake Mratibu wa uchaguzi wa Mkoa wa Ruvuma Salum Kateula amesema lengo la kikao hicho ni kupitia maeneo muhimu yanayohusu kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mwaka 2024.

Ameongeza kuwa wananchi wanaendelea kuelimishwa kuhusu uchaguzi kwa kutumia mabango, matangazo, matamasha, na vikao mbalimbali katika ngazi za Wilaya, kata, na vijiji ambapo Elimu hiyo inalenga kuwawezesha kujiandikisha katika daftari la wapiga kura na kuelewa mchakato mzima hadi siku ya uchaguzi.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mara ya mwisho ulifanyika tarehe 24 Novemba, 2019 ambapo mwaka huu uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba.

Baadhi ya wadau wa uchaguzi wa Mkoa wa Ruvuma wakiwa kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.