• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA kituo cha pili kwa ukubwa uzalishaji mbegu bora nchini

Imewekwa kuanzia tarehe: April 29th, 2024

Na Albano Midelo

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed ameipongeza serikali kupitia Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) kwa kuuwezesha Mkoa kuwa kituo cha pili kwa ukubwa hapa nchini kwa uzalishaji wa mbegu bora.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya mkulima yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya shamba la mbegu Namtumbo linalomilikiwa na ASA,Kanali Abbas  amelitaja shamba hilo la kuzalisha mbegu kuwa ni la pili kwa kubwa nchini likiwa na hekta 3,580.4.

“Hii ni fursa kubwa kwetu tulioendelea kupewa na Taifa,licha ya Mkoa wa Ruvuma kuwa wazalishaji wa kwanza nchini wa mazao ya chakula  na nafaka ,bado Mkoa umeendelea kupata heshima ya kuwa ni kituo cha uzalishaji mbegu wa mbegu bora cha pili kwa ukubwa ndani ya Taifa letu’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Ameipongeza Wizara ya Kilimo kwa kuamua kulirudisha shamba la NAFCO Namtumbo kuwa miongoni mwa mashamba ya serikali yanayozalisha mbegu bora ambazo zitaongeza uzalishaji mazao ya chakula  na serikali kujihakikishia usalama wa chakula.

Ameongeza kuwa mbegu bora zinazozalishwa kwenye kituo hicho zitapatikana kwa gharama nafuu na kwamba mradi huo umetoa fursa kwa wawekezaji wa kilimo cha mkataba ambapo ameiagiza ASA kuhakikisha wanapatikana wawekezaji wengi wa mkataba ili shamba hilo lisibaki kuwa mapori.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ametoa rai kwa ASA kuhakikisha wanafanya kilimo cha kisasa kwa kuondokana na kilimo cha matumizi ya vifaa duni badala yake kuongeza kasi ya kutumia vifaa vya kisasa.

Hata hivyo amesema licha Mkoa kufanya vizuri kwenye kilimo,bado Mkoa unaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe na kuwepo vivutio vikubwa vya utalii vinavyoupambanua Mkoa .

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo  (ASA) Dkt.Sophia Kashenge akizungumza kwenye maadhimisho hayo amelitaja shamba la mbegu Namtumbo lenye ukubwa wa hekta 3,580.4 kuwa ni miongoni mwa mashamba 16 ya mbegu yenye jumla ya hekta 17,710.26.

Ameyataja mashamba hayo ya mbegu yanapatikana katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Ruvuma, Tanga, Pwani, Arusha, Tabora, Kigoma,Katavi na Geita na kwamba shamba la mbegu Namtumbo ni la pili kwa ukubwa hapa nchini likiwa na watumishi 15.

Amesema katika msimu  wa mwaka 2023/2024,shamba la mbegu Namtumbo linatarajia kuzalisha mbegu Zaidi ya tani 1,275 za mazao mbalimbali yakiwemo mahindi na alizeti .

Amelitaja shamba la mbegu Namtumbo kuwa limetoa mchango mkubwa wa kukabiliana na upungufu wa chakula katika mikoa mingine ikiwemo wilaya ya Nzega Mkoa wa Tabora na Wilaya ya Hanang Mkoa wa Manyara .

Kulingana na Dkt. Kashenge, mikakati ya shamba hilo ni kuongeza uzalishaji wa mbegu za mafuta hasa alizeti na ufuta ili kuongeza uzalishaji wa mafuta ya kula na kupuguza uagizaji wa mafuta toka nje ya nchi hali ambayo itapunguza matumizi ya fedha za serikali katika kuagiza mafuta hayo nje.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya ameitaja Wilaya hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuufanya Mkoa wa Ruvuma kuwa ghala la chakula nchini ambapo katika msimu uliopita wilaya ilizalishaji mahindi Zaidi ya tani 1,552,955 na kwamba msimu huu Wilaya inatarajia kuzalisha mahindi Zaidi ya tani 1,920,550.

Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) ulianzishwa chini ya sheria ya Wakala za Serikali namba 30 ya mwaka 1997 lengo kuu likiwa ni kuongeza uzalishaji na upatinaji wa mbegu bora kwa wakulima kwa bei nafuu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.