• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

Ruvuma Kuimarisha Mapambano Dhidi ya UKIMWI

Imewekwa kuanzia tarehe: December 2nd, 2018

Ruvuma Kuimarisha Mapambano Dhidi Ya UKIMWI-RC Mndeme


Tunduru.



Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amezitaka taasisi na wadau wa mapambano dhidi ya UKIMWI kuongeza jitahada za kuzuia maambukizi mapya kuongezeka.


Ametoa agizo hilo Leo (Jumamosi tarehe 01.Desemba,2018) katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa Baraza la Idd wilaya ya Tunduru.


Akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu huyo wa Mkoa,Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera amesema takwimu zinaonyesha Ruvuma ina kiwango cha maambukizi ya VVU/UKIMWI cha asilimia 5.6 zaidi ya kile cha Taifa cha asilimia 4.7 kwa mwaka 2016/2017.


Takwimu hizi ingawa zinaonekana kushuka kwa kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 7 mwaka 2011/2012 bado kunahitajika nguvu na mikakati mipya ya kushusha zaidi kiwango cha maambukizi ya VVU.


Ili kuhakikisha maambukizi mapya yanapungua Mndeme amesisitiza mkakati wa upimaji wa hiari wa VVU uimarishwe kwenye wilaya zote tano.


Ameongeza kusema ni wakati sasa kuhakikisha watu wote wanaokutwa na VVU wanaanzishiwa tiba mara moja.


Mkuu wa wilaya Homera ameishukuru serikali ya awamu ya Tano kwa kuongeza bajeti ya dawa hadi kufikia Shilingi Bilioni1.3 kwa mkoa wa Ruvuma kufikia mwezi Juni 2018 ikilinganishwa na shilingi milioni 297.5 zilizotolewa mwaka 2016/2017 kwenda Bohari Kuu ya Dawa (MSD).


Mafanikio haya amesema yamesaidia wananchi wengi wa mkoa wa Ruvuma kuwa na uhakika wa matibabu hivyo kuongeza jitihada za kupunguza kasi ya maambukizi ya VVU.


Kwa upande wake Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt.Magdalena Zenda amesema katika kipindi cha Januari hadi Octoba 2018 jumla ya wananchi 456,777 walipimwa hali zao za maambukizi.


Kati yao waliogundulika na maambukizi ni 8,494 ambapo wanaume walikuwa (3,764) na wanawake (4,730).


Dkt .Zenda ameongeza kusema hadi kufikia mwezi Octoba 2018 Mkoa umefanikiwa kusajili na kuanzisha dawa za kufubaza Virusi (ARV) kwa WAVIU 63,671 tangu huduma hizi zianze mwaka 2004.


"Kati yao wanaotumia dawa hadi sasa ni 42,056 ,wanaume ni (14,336) na wanawake (27,720) wanaendelea kupata huduma katika kliniki za tiba na matunzo (CTC) kote mkoani " alisema Dkt.Zenda.


Ametaja changamoto kubwa ni idadi ya wanaotumia ARV wapatao 14,899 kuhamia vituo vingine nje ya mkoa na 11,368 ni waVVU waliopoteza ufuasi.


Katika kipindi cha mwaka 2004 hadi sasa mkoa umekuwa na vifo vitokanavyo na UKIMWI 7,168 .


Mkoa wa Ruvuma wenye watu takribani 1,449,830 kwa sensa ya mwaka 2012 una vituo vya kutolea huduma za afya 314.


Kati yake hospitali zipo (11),vituo vya afya (32) na zahanati (271) hii inafanya huduma za upimaji na matibabu ya VVU kupatikana karibu maeneo yote.


Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya UKIMWI mwaka huu 2018 inasema " Know your status" -Pima,Jitambue,Ishi.

Mwisho.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.