• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUVUMA yazindua programu ya uhifadhi misitu

Imewekwa kuanzia tarehe: December 14th, 2023

Viongozi wa Taasisi za dini mkoani Ruvuma wahimizwa kutoa elimu kwa jamii umuhimu wa kuhifadhi mazingira ili kupunguza athari za mabaliko ya tabia ya nchi.

Wito huo umetolewa na Afisa maliasili Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe wakati wa uzinduzi wa progamu ya uhifadhi misitu na mazingira iliyoandaliwa na shirika la utunzaji wa mazingira duniani (WWF)

Challe amesema kuwa Viongozi wa dini wanao wajibu wa kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu kupitia mafundisho ya dini kwa kutumia sera mazingira ya mwaka 2022 ili malengo yaliyowekwa na Serikali katika sekta ya uhifadhi mazingira yanatimia.

“Viongozi wadini ni watu ambao wanasikilizwa sana na waumini zao kwahiyo kupitia wao tumeona tuwaharike kama wadau kwa lengo la kuwahimiza na kuwasisitiza juu ya uhifadhi wa upandaji miti ili kuboresha mazingira kwasababu wanamchango mkubwa kwa jamii ”alisema Challe.

Pia amesema katika kusisitiza utunzaji wa mazingira katika mkoa wa Ruvuma  kila ifikapo mwezi januari ufanya kampeni ya upandaji miti mkoa mzima kwa kutoa miche laki tatu  ambayo utolewa na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake mratibu wa progamu za mazingira, utunzaji wa misitu na upandaji miti mkoa wa Ruvuma Ndugu Furuko Hyera amesema progamu hiyo inalenga kutunza aridhi na kupunguza athari za mabaliko ya tabia nchi.

Amesema kupitia programu hiyo itasahidia kufundisha jamii kuhusu kurithisha kwa vizazi kuhusu utunzaji mazingira kwa kupanda miti kuliko kurithisha uvunaji miti holela ambao umekuwa ukisababisha majanga kama vile ukame, mafuriko ambapo athari za majanga hayo hayachagui dini bali yanakuja kwa wote.

“Programu hii itaenda kufundisha jamii kuwa itambue kuwa pale inapotaka au kuvuna miti itambue kwamba wanapovuna miti watambue kunawalioipanda na kuiotesha hivyo jamii inatakiwa kuwa na mazoea kufundisha watoto kupanda miti ili kizazi kijacho kiweze kunifaika na utunzaji mazingira na upandaji miti wa sasa”amesema Hyera

Naye Shekhe wa Mkoa wa Ruvuma Ramadhani Mwakilima amesema anaishukuru shirika la utunzaji wa mazingira duniani (WWF) kwa kutambua mchango wa viongozi wa dini katika kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa misitu

“Sisi kama viongozi wa dini tumelipokea na tumejipanga kuzungumza na kuwahasmisha waumini wetu pia kama taasisi za dini hatuwezi kujitenga na umuhumu wa kuhifadhi na kutunza mazingira” amesema Mkilima.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.