• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUWASA washusha neema Gereza la Kitai

Imewekwa kuanzia tarehe: August 31st, 2023

ZAIDI ya wakazi 1,464 wa Kitai na Ngembambili wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,wanatarajiwa kuondokana na kero ya uhaba wa maji safi na salama baada ya wakala wa usambazaji maji na usafi wa mazingira(RUWASA)kuanza ujenzi wa mradi mkubwa wa maji utakaogharimu zaidi ya Sh.milioni 560.

Mkuu wa Gereza la Kitai Mrakibu wa Magereza Gabriel Rudeligo amesema,kero ya maji safi na salama ni ya muda mrefu kutokana na kukosekana kwa chanzo cha uhakika hivyo kupelekea wakazi wanaoishi katika eneo hilo wakiwemo askari na familia zao kulazimika kutumia maji ya visima vya asili na mito ambayo siyo safi na salama.

Rudeligo,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kutoa fedha kwa wizara ya maji na Ruwasa kuanza ujenzi wa mradi huo ambao ukikamilika utamaliza kilio cha muda mrefu cha ukosefu wa maji safi na salama iliyokuwepo tangu Uhuru.

Amesema,kila siku katika eneo la Gereza kuna mkusanyiko mkubwa wa watu hasa wafungwa,wanafunzi wa shule ya msingi,wananchi wanaofika kupata huduma za matibabu kwenye zahanati na familia za askari ambao wanahitaji huduma ya maji ya uhakika kwa ajili ya matumizi ya kila siku .

Mkuu wa Gereza amesema,ni faraja kubwa kama kiongozi wa eneo hilo kuona kilio cha maji sasa kinakwenda kumalizika na kuwapongeza wataalam wa Ruwasa wilaya ya Mbinga na mkoa kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.

Ameongeza kuwa,pindi mradi huo utakapo kamilika utawaondolea adha na kero kubwa ya kwenda kutafuta maji kwenye vyanzo vya asili ambavyo havikutosheleza mahitaji yao,hali iliyosababisha baadhi ya shughuli za uzalishaji mali kufanyika kwa kusua sua licha ya nguvu kazi kubwa waliyonayo.

Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa usambazaji maji na usafi wa mazingira(RUWASA)Mhandisi Ruth Koya,amewataka wananchi wanaoishi katika eneo hilo na maeneo ya jirani kuhakikisha wanatunza mradi huo ili uweze kudumu kwa muda mrefu na kuwa suluhisho la changamoto ya maji kwao.

Aidha,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia fedha Ruwasa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji ikiwemo mradi wa maji Kitai ambao unakwenda kutimiza dhamira yake ya kumtua mama ndoo kichwani.

Meneja wa RUWASA wilaya ya Mbinga Mhandisi Mashaka Sinkala alisema,mradi wa maji Kitai utahudumia takribani wakazi 1,468 kati yao 1,204 ni kutoka Gereza la Kitai,shule ya msingi na Zahanati na wakazi 264 kutoka Kitongoji cha Ngembambili ambacho ni maarufu kwa uchimbaji wa madini.Amesema,mradi huo unatekelezwa kwa kutumia wataalam wa ndani na ulianza kutekelezwa mwezi Februari 2023 na ulitakiwa kukamilika mwezi Juni,lakini muda wa utekelezaji wake uliongezwa hadi mwezi Septemba kutokana na sababu za mvua kubwa zilizonyesha na mwingiliano wa kazi hususani za uchimbaji wa mitaro ambazo zilizofanywa na wafungwa wa gereza hilo.

Amelitaja lengo kuu la mradi huo ni kutoa huduma ya maji kwa jamii inayoishi katika eneo na ndani ya gereza la kitai ambalo lilikuwa na uhaba mkubwa wa maji ambapo ukikamilika utasaidia sana kupunguza magonjwa ya mlipuko na kutoa fursa kwa jamii kupata muda wa kushiriki shughuli mbaimbali za kiuchumi.

Amesema,mradi huo utagharimu zaidi ya Sh.milioni 560 na hadi sasa fedha zilizotumika ni Sh.321,710,650.44 sawa na asilimia 57.4 ambazo zimetumika kwa kununua mabomba,tenki na vifaa vingine vya kujengea.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.