• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUWASA yatekeleza mradi wa maji wa milioni 50 katika kijiji cha Chimate Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: June 24th, 2020

SERIKALI ya awamu ya tano imetoa sh.milioni 50 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji kwenye kitongoji cha  Mingohi kijiji cha Chimate Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.


Akisoma taarifa ya  mradi  huo, kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme alipokagua mradi huo,Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) Wilaya ya Nyasa Mhandisi Evaristo Ngole amesema utekeleza wa mradi huo umefikia asilimia 90 ambapo hadi sasa zimetumika zaidi ya sh.milioni 43.


Mhandisi Ngole amesema mradi ulianza kutekelezwa Februari mosi mwaka huu na kwamba  kulikuwa na mikataba mitatu ya Utekelezaji wa mradi huo ikiwemo ujenzi wa tanki lenye mita za ujazo  25,000 kwenye chanzo cha maji kwenye milima ya Livingstone.


‘’ Mradi unatekelezwa kwa fedha za  wadau wa maendeleo kutoka nchini Uingereza ambao hutoa fedha kupitia Wizara yetu ya Maji chini ya Mpango wa Lipa kutokana na matokeo’’,alisisitiza Ngole.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba amesema serikali imetoa  zaidi ya sh.milioni 390 za kujenga mradi wa maji katika vitongoji vitatu vilivyobaki vya kijiji cha Chimate ambavyo ni Mtakanini,Chimate kati na Chiwanda.


Amesema tangu kuanzishwa kwa RUWASA  Wilaya ya Nyasa imeendelea kutekeleza miradi chini ya program ya maendeleo ya sekta ya maji awamu ya pili ambapo kupitia program hiyo,miradi inatekelezwa kwa fedha za mpango wa lipa kutokana na matokeo.


Akizungumza baada ya kukagua mradi huo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema ameridhika na Utekelezaji wa mradi wa maji katika kitongoji cha Mingohi ambao amesema umewaondolea kero wananchi ya kutumia muda mrefu kwa kutembea umbali mrefu kutafuta maji.



‘Mradi wa milioni 50,wanakwenda kufaidika wananchi  zaidi ya 1200 kwa kujengewa vituo 12 vya kuchota maji katika  kitongoji cha Mingohi ambacho tangu nchi yetu ipate uhuru  hawajawahi kupata maji ya bomba,tuna kila sababu ya kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu’’,alisisitiza Mndeme.


Tangu serikali ya awamu ya tano imeingia madarakani kwa Mkoa wa Ruvuma pekee  imetoa zaidi ya shilingi bilioni 30 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji  hali ambayo imewaondolea kero wananchi ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Imeandailiwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma 

Nyasa 

Juni 22,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.