• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RUWASA yatumia zaidi ya shilingi bilioni 2.5 kutekeleza miradi mitatu ya maji Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: September 3rd, 2023

WAKALA wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma imetumia zaidi ya shilingi bilioni 2.5 kutekeleza miradi mitatu ya maji.

Meneja wa RUWASA wilayani Mbinga Mhandisi Mashaka Sinkala ameitaja miradi hiyo kuwa ni Pamoja na mradi wa maji Kitai ambao hadi kukamilika unatarajia kutumia shilingi milioni 560.

Amesema mradi huo utahudumia jumla ya wakazi 1,468 kati yao wakazi 1,204 wanatoka katika Gereza la Kitai,shule ya msingi Kitai na zahanati ya Kitai na kwamba wakazi 264 wanatoka katika kitongoji cha Ngembambili.

Mhandisi Sinkala ameutaja mradi mwingine ambao unatekelezwa na RUWASA kuwa ni mradi wa maji kata ya Matiri ambao unagharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.4

Ameutaja mradi wa maji Matiri kuwa unahusisha vijiji vya Matiri na Kiyaha na kwamba mradi unatarajia kuhudumia wakazi zaidi ya 9870.

Hata hivyo amesema mradi huo hadi sasa umefikia asilimia 60 ya utekelezaji na unatarajia kukamilika Novemba 17 mwaka huu ambapo amesisitiza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutapunguza adha kubwa ya upatikanaji wa maji iliyokuwepo kabla ya kuanza kutekelezwa mradi huo.

“Wananchi wa Matiri kwa muda mrefu wamekuwa wanasumbuliwa na magonjwa ya milipuko kutokana na kutumia maji ambayo sio salama,mradi huu pia utasaidia watu kupata muda mwingi wa kushughulika na kazi zingine za kiuchumi kwa kuwa maji yatakuwa karibu na makazi’’,alisisitiza.

Mradi mwingine ambao unatekelezwa na RUWASA  wilayani Mbinga kulingana na Meneja huyo ni mradi wa maji Kitanda unaohusisha vijiji vya Kitanda na Magwangala na kwamba mradi unatarajia kuhudumia jumla ya wakazi 3,600.

Amesema mradi huo unatarajia kutumia zaidi ya shilingi milioni 473  na kwamba mradi  umekamilika kwa asilimia 100 na unakwenda kupunguza adha kubwa ya upatikanaji wa maji kwenye vijiji husika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa RUWASA Tanzania Mhandisi Ruth Koya ameitaja azma ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kichwani inakwenda kutimia miaka michache ijayo.

Amesema anaamini kufikia mwaka 2025 asilimia 85 ya wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini watakuwa wanapata maji safi na salama.

Ameiagiza Menejimenti ya RUWASA kuhakikisha kwamba wakandarasi wanaoidai serikali fedha walipwe mara moja kwa kuwa serikali imeshatoa fedha za kutekeleza miradi hiyo kilichobakia ni taratibu za kuwalipa zikamilike haraka ili wakandarasi wakamilishe kazi zao.

Kaimu Mkurugenzi wa RUWASA Bwai Biseko amesema RUWASA haitaki kujisifia kwa kuhesabu miradi mingapi imetekelezwa badala yake wanapenda kuona namna walivyowagusa  wananchi kuhakikisha mradi umekamilika na wananchi wanapata huduma.

Stella Mhagama Mkazi wa Matiri amesema anamshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi huo ambapo amesema kwa miaka mingi wanawake na Watoto wamekuwa wanapata kero ya kusafiri kilometa nne kufuata maji mtoni na kubeba kichwani.

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imetoa zaidi ya shilingi bilioni 58 katika Mkoa wa Ruvuma kutekeleza miradi 36 ya maji hadi kufikia Juni 30 mwaka huu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.