• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SEKONDARI mpya tisa za SEQUIP Ruvuma zinavyovutia wanafunzi

Imewekwa kuanzia tarehe: February 19th, 2024

Na Albano Midelo,Songea

SHULE mpya tisa za sekondari  zilizojengwa mkoani Ruvuma kupitia Program ya Uboreshaji Elimu ya Sekondari (SEQUIP) kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni tano  zimekamilika na kuanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka huu.

Serikali kupitia SEQUIP awamu ya pili katika mwaka 2022/2023 imetoa zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa sekondari mpya za kata 176 kati ya hizo sekondari tisa zimejengwa mkoani Ruvuma,

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ametoa fedha hizo ili kujenga shule mpya za sekondari za kata katika kata zisizo na shule na kata zenye wanafunzi wengi zaidi ukilinganisha na miundombinu ya shule zilizopo.

Wanafunzi  walioanza masomo katika sekondari hizo mkoani Ruvuma wameipongeza serikali kwa kuwajengea sekondari hizo ambazo zimemaliza changamoto ya wanafunzi kusafiri umbali mrefu kufuata sekondari.

Juma Issa na Khadija Kassim  ni wanafunzi wa sekondari mpya Kata ya Tinginya wilayani Tunduru ambayo wamesema kabla ya ujenzi wa sekondari hii,wanafunzi waliofaulu katika Kata hiyo walikuwa wanakwenda kusoma katika sekondari ya Nakapanya ambayo ipo umbali wa kilometa 40.

“Kutokana na umbali huo wanafunzi wengi waliacha shule,utoro ulikuwa mwingi na Watoto wa kike walipata mimba baada ya kukumbwa na vishawishi vingi’’,alisema Khadija Kassim.

Mariam Ismail ni Mwananchi kutoka Kijiji cha Tinginya amesema kabla ya sekondari hiyo wazazi walipata gharama kubwa kwa Watoto wao ikiwemo nauli ya kusafiri Kwenda sekondari ya Nakapanya ambapo baadhi ya wazazi walishindwa kumudu ambapo hivi sasa wanamshukuru Rais kwa kuwajengea sekondari hiyo.

Mkuu wa sekondari ya Tinginya Romatus Ndoa amesema walipokea kiasi cha shilingi milioni 560 ambazo zimetumika kujenga jengo la utawala,madarasa manane,vyumba vitatu vya maabara,jengo la TEHAMA,kichomea taka,minara miwili ya maji na vyoo matundu 12,

Amesema wanafunzi wameanza masomo tangu Januari mwaka huu ambapo sekondari hiyo ya kisasa na mazingira ya kuvutia imeondoa kabisa changamoto ya wanafunzi wa Kata ya Tinginya kusafiri umbali mrefu.

Teresia Ng’ombo ni Kaimu Mkuu wa shule ya sekondari Tuwemacho wilayani Tunduru ambaye amesema wamepokea wanafunzi  70 kati ya 87 waliopangiwa kuanza kidato cha kwanza katika sekondari hiyo.

Zamda Yusufu na Siyawezi Libadi ni wanafunzi wa kidato cha kwanza katika sekondari ya Tuwemacho   wamesema ujenzi wa sekondari hiyo umemaliza tatizo la wanafunzi kusafiri kilometa 45 hadi sekondari ya Namasakata kufuata shule.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa shule ya sekondari Mputa wilayani Namtumbo  Filbert Mbunda  amesema sekondari hiyo imepokea wanafunzi wa kidato cha kwanza wapatao 157 kati yao waliomaliza darasa la saba mwaka 2023 ni 135 na waliomaliza darasa la saba mwaka 2022 ni 22.

Amesema kabla ya kuanza sekondari hiyo wanafunzi wote waliokuwa wanafaulu darasa la saba walipelekwa sekondari ya Mbunga iliyopo Kata ya Kitanda ambapo walikuwa wanatembea umbali wa kilometa 30 kila siku hali iliyosababisha wanafunzi wengi kuacha shule.

Naye Mkuu wa shule ya sekondari ya Lilondo Subira Mapunda amesema  baada ya shule hiyo kukamilika wamepokea wanafunzi wa kidato cha kwanza ambao walikuwa wanasafiri umbali wa kilometa 20 hadi sekondari ya Wino ambapo hivi sasa wanafunzi wanafurahia mazingira mazuri ya kujifunzia.

Ado Kawonga ni Kaimu Mkuu wa sekondari ya Mtopesi iliyojengwa katika Kijiji cha Lugagara Halmashauri ya Wilaya ya Songea amesema mara baada ya kukamilisha ujenzi wamepokea wanafunzi 71 wa kidato cha kwanza hivyo kumaliza changamoto ya wanafunzi kutembea kilometa 30 kila siku kufuata sekondari ya Kilagano.

Petro Liweli ni Mkuu wa shule ya sekondari ya Dkt.Lawrence Gama iliyopo Kata ya Mkuzo Manispaa ya Songea  amesema wamepokea jumla ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 200 ambao wameanza masomo mwaka huu .

Katika Programu ya SEQUIP Awamu ya kwanza Mkoa wa Ruvuma  ulitengewa zaidi ya shilingi bilioni 7.7 kujenga sekondari mpya za kata 11 ikiwemo sekondari moja ya Mkoa kwa ajili ya Watoto wa kike ambayo imejengwa wilayani Namtumbo na imeanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha Tano mwaka 2023. na wanafunzi w kidato cha kwanza 2024.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.