• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI ilivyodhamiria kuifungua wilaya ya Nyasa kwenye miundombinu

Imewekwa kuanzia tarehe: August 2nd, 2023

SERIKALI  imetenga shilingi bilioni 22 kuanza kujenga daraja la Mitomoni katika mto Ruvuma linalounganisha wilaya ya Nyasa na Songea  mkoani Ruvuma.

Haya yamesemwa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Gofrey Kasekenya wakati anazungumza na wananchi wa Mji wa Mbambabay wilayani Nyasa.

Amesema tayari serikali imelisanifu daraja la mitomoni na Mkandarasi ameshapatikana na kwamba ujenzi wa daraja hilo unatarajia kuanza mwaka huu wa fedha.

Amesema kutokana na umuhimu wa barabara ya Nangombo hadi Chiwindi mwambao mwa ziwa  Nyasa mwaka huu serikali  imeingiza barabara hiyo kwenye utaratibu wa  kufanyiwa upembezi yakinifu na usanifu wa kina.

Hata hivyo amesema barabara ya Mbambabay hadi Lituhi tayari imefanyiwa usanifu wa kina ili hatimaye ianze kujengwa kutokana na umuhimu wa barabara hiyo ambayo ni ya ulinzi na inaunganisha Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Njombe.

Hata hivyo amesema tayari serikali imeifungua wilaya ya Nyasa kwa kujenga barabara ya lami nzito kilometa 66 kutoka Mbinga hadi Mbambabay iliyogharimu zaidi ya shilingi bilioni 129 na serikali ya Awamu ya Sita imekamilisha daraja la mto Ruhuhu lenye urefu wa meta 100 linalounganisha wilaya ya Nyasa Mkoa wa Ruvuma na wilaya ya Ludewa mkoani  Njombe.

Amesema serikali pia inaendelea kujenga barabara ya Lami  kipande cha kutoka Kitahi wilayani Mbinga hadi Ndumbi wilayani Nyasa ambako imejengwa bandari ya Ndumbi ambayo imekamilika kwa asilimia 100 na imejengwa shilingi zaidi ya bilioni 12.

“Barabara ya Kitai hadi Ruanda kwa kiwango cha lami inaendelea kujengwa,pia serikali itaendelea kujenga barabara ya lami kutoka Ruanda-Lituhi hadi Ndumbi,Mkandarasi ameshapatikana barabara hiyo inaanza kujengwa kwa kiwango cha lami mwaka huu wa fedha’’,alisema Mhandisi Kasekenya.

Ameongeza kuwa serikali katika mwaka huu wa fedha imetoa shilingi bilioni 70 ili kuanza kujenga upya bandari ya Mbambabay wilayani Nyasa hali ambayo itaiunganisha wilaya ya Nyasa  na nchi jirani za Malawi na Msumbiji kupitia ziwa Nyasa.

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Filberto Sanga ameishukuru serikali kwa kuifungua wilaya ya Nyasa kwa njia ya barabara na majini hali ambayo imemaliza kero ya usafiri na usafirishaji

Amesema Wilaya ya Nyasa imefunguka kupitia ziwa Nyasa,serikali imejenga meli tatu mpya moja ya abiria inayoitwa MV Mbeya II na meli mbili za mizigo zinazoitwa MV Njombe na MV Ruvuma zinazofanya kazi katika ziwa Nyasa kupitia bandari za wilaya ya Kyela  Mkoa wa  Mbeya,Ludewa Mkoa wa Njombe na Nyasa Mkoa wa Ruvuma.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.