• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI kushughulikia changamoto za wazee

Imewekwa kuanzia tarehe: September 21st, 2022

Madiwani waagizwa kusimamia miradi

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema serikali itaendelea kutafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wazee zikiwemo kutoa vitambulisho vya matibabu bure kwa wazee.

Kanali Thomas ametoa ahadi hiyo wakati anazungumza na wazee Pamoja na madiwani  wa Wilaya ya Mbinga kwa nyakati tofauti katika ukumbi wa sekondari ya Kigonsera na sekondari ya Makita mjini Mbinga.

RC Thomas ametoa rai kwa wazee kuhakikisha changamoto zote zinazowakabili wanazifikisha kwenye Baraza la Wazee la Mkoa wa Ruvuma ambalo limezinduliwa hivi karibuni ili ziweze kutatuliwa kwa haraka.

“Serikali ya Awamu ya Sita ipo tayari kusikiliza na kushughulikia kero mbalimbali za wazee,pia nawaasa vijana hakikisheni mnawahudumia wazee wenu ili mpate baraka kwa sababu wazee ni kudni muhimu ambalo limesahaulika katika jamii ’’,alisisitiza Kanali Thomas.

Ameagiza huduma za afya kuboreshwa katika dirisha la kuhudumia wazee katika kila kituo cha kutolea huduma za afya ili wazee waweze kupata huduma za matibabu kwa haraka.

Mkuu wa Mkoa pia amewaasa wazee kutumika kutatua migogoro inayojitokeza katika jamii na kwamba wazee wanatakiwa kuwa washauri wakuu katika jamii hali ambayo italeta amani na utulivu na vijana kupata fursa ya kujifunza kutoka kwa wazee.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaagiza madiwani wa Halmashauri zote kuwa walinzi wa miradi inayotekelezwa katika Kata zao ili iweze kukamilika kwa wakati na ubora unaolingana na thamani ya fedha zilizotumika kwenye miradi husika.

Ameagiza viporo vya miradi ambayo haijakamilika kwa muda mrefu kuhakikisha wanaisimamia na inakamilika ndani ya muda mfupi ili wananchi waanze kunufaika na miradi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mheshimiwa Aziza Mangasongo akitoa taarifa ya wazee kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,alisema Halmashauri ya Mbinga imewatambua wazee zaidi ya 19,000 hadi kufikia Julai mwaka huu.

Mangasongo amesema wilaya hiyo imeendelea kuwatambua wazee na kutoa vitambulisho vya matibabu kwa wazee ambapo hadi sasa tayari vitambulisho vya CHF iliyoboreshwa vimetolewa katika kaya 4824 zilizojiunga na CHF kati ya kaya zaidi ya 57,000 zilizopo.

Awali wazee wa wilaya ya Mbinga  akiwemo mzee Filo Mbepera,Deotela Ndunguru,Anasitazia Hyer ana Emilian Mapunda walizitaja changamoto kuu zinazowakabili wazee na kuiomba serikali kuzipatia ufumbuzi kuwa ni idadi ndogo ya wazee waliopo kwenye mpango wa kaya masikini (TASAF) hivyo kuomba serikali kuongeza idadi ya wazee wanaonufaika na TASAF.

Changamoto nyingine walizitaja kuwa  ukosefu wa dawa muhimu za matibabu kwa wazee,baadhi ya wastaafu kuchelewa kupata kiinua mgongo baada ya kustaafu na baadhi ya wazee kuwa hatarini kupoteza maisha kutokana na Imani za kishirikina.

RC Thomas anaendelea na ziara ya kuzungumza na wazee katika wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma ambapo tayari amezungumza na wazee wa wilaya za Namtumbo na Mbinga.

Imeandikwa  na Albano Midelo

Afisa Habari Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ruvuma

Septemba 20,2022

 

  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.