• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa bilioni sita kutekeleza miradi Songea,RC akagua atoa maagizo

Imewekwa kuanzia tarehe: June 28th, 2023

SERIKALI imetoa zaidi ya shilingi bilioni sita kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma katika mwaka wa fedha wa  2022/2023.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Neema Maghembe wakati anatoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alipofanya ziara ya ukaguzi wa miradi katika Halmashauri hiyo.

Maghembe amebainisha kuwa kati ya fedha hizo,Halmashauri imepokea zaidi ya shilingi milioni 735 kwa ajili ya mradi wa uboreshaji miundombinu ya awali na msingi (BOOST),mradi wa vyoo (SWASHI) zimetolewa  zaidi ya shilingi milioni 278 na na mradi wa ujenzi wa madarasa ya awali ya mfano (LANES) zimetolewa zaidi ya shilingi milioni 55.

“Halmashauri inapenda kuishukuru serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa namna inavyoendelea kuleta fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri yetu’’,alisema Maghembe.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo,Halmashauri hiyo pia imepokea  zaidi ya shilingi milioni 637 kwa ajili ya umaliziaji wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi,zaidi ya shilingi milioni 75 kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi ya maendeleo vijijini na kwamba serikali pia imetoa shilingi milioni 440 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi.

Kulingana na Mkurugenzi huyo,serikali imetoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya msingi Lizabon na shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa na vyoo.

Fedha nyingine zilizotolewa na serikali katika Halmashauri hiyo ni zaidi ya shilingi milioni 155 ambazo zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya walimu,zaidi ya shilingi milioni 142 kwa ajili ya ujenzi wa bweni sekondari ya Darajambili na chuo cha ufundi Liganga.

Maghembe amezitaja fedha nyingine zilizotolewa ni zaidi ya shilingi milioni 278  kwa ajili ya ujenzi wa vyoo shule za msingi,zaidi ya milioni 362 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa,mabweni na vyoo,milioni 834 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 12,mabweni na vyoo .

Amesema serikali pia imetoa zaidi ya shilingi milioni 751 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ,mabweni na matundu ya vyoo katika sekondari ya Mpitimbi na shilingi bilioni moja zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha wenye ulemavu Kata ya Liganga.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amekagua mradi wa vyoo katika shule ya msingi Parangu uliogharimu shilingi milioni 37,mradi  wa  ukarabati Kituo cha Walimu (TRC) cha Peramiho kilichogharimu shilingi milioni 22 na mradi wa vyumba vya madarasa ya awali yaliyogharimu shilingi milioni 61 katika Kijiji cha Mpitimbi.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa miradi hiyo,Mkuu wa Mkoa  wa Ruvuma amepongeza mradi wa ujenzi wa madarasa ya awali katika Kijiji cha Mpitimbi ambapo ametoa rai kwa wananchi  kulinda na kusimamia mradi huo ili uweze kukamilika kwa asilimia 100.

Hata hivyo Kanali Laban hajaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya vyoo katika shule ya Parangu na ukarabati wa Kituo cha walimu Peramiho ambapo ameiagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi wa kina katika miradi hiyo na kuchukua hatua kwa mtumishi yeyote atakayebainika kuwa na kosa.

Amewataka viongozi kuanzia ngazi ya Kijiji,Kata,Tarafa na Wilaya kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali badala ya kusubiri ziara za viongozi wa Mkoa kufutilia miradi hali inayosababisha miradi kutekelezwa chini ya kiwango.

Amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Neema Maghembe kuwaandikia barua ya onyo na hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa waandisi wote wanaosimamia miradi kwa sababu wameshindwa kusimamia miradi.  

Mwisho

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.