• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa milioni 470 kujenga sekondari ya Mndeme Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: February 12th, 2023

SERIKALI imetoa Sh.milioni 470  kujenga shule mpya ya sekondari  katika kijiji cha Amani-Makolo kata ya Amani-Makolo Halmashauri ya wilaya Mbinga mkoani Ruvuma, ili kumaliza kero ya wanafunzi wanaotoka katika kata hiyo kwenda kata ya Mkako umbali wa km 15 kufuata masomo

Awali wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi  katika kata hiyo na kuchaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza walilazimika kwenda kata nyingine kama vile Mkako,Rwanda na wengine hata shule zilizopo Mbinga mjini kwa ajili ya kuanza  masomo ya sekondari.

Kaimu Afisa elimu sekondari wa Halmashauri hiyo Rashid Bundala amesema,kujengwa kwa shule hiyo ni ukombozi mkubwa hata kwa wazazi ambao walilazimika kuwalipia watoto wao gharama ya kusafiri kwenda shule na kurudi nyumbani kila siku.

Amesema,baadhi ya wanafunzi wanaotoka vijiji vya kata hiyo walilazimika kupanga vyumba uraini na kuanza kujitegemea licha ya umri mdogo walionao

Bundala alieleza kuwa,kutokana na changamoto hiyo baadhi ya watoto hasa wa kike walishawishika kuanza mahusiano ya kimapenzi na watu wazima wasiokuwa na maadili mema na hatimaye kushindwa kumaliza masomo kwa kupata mimba na wengine kuchoshwa na umbali uliopo.

Aidha amesema,ujenzi wa shule ya Sekondari Mndeme ni utekelezaji wa Ilani ya  uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi inayotaka kila kata kuwa na shule ya sekondari ili vijana wengi wanaomaliza darasa la saba wapate  nafasi ya kuendelea na elimu ya sekondari.

Amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,kutoa fedha ili kujenga shule hiyo sekondari  ambayo ni msaada mkubwa kwa watoto wa kata ya Amani-Makolo ambao sasa wanatoka nyumbani na kwenda shule iliyopo karibu na makazi yao.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mndeme,wameishukuru serikali kuwajengea shule mpya na kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kwenda katika kata nyingine kufuata masomo.

Solana Adam amesema,wanafunzi wanaotoka katika kijiji hicho walikuwa wakitembea  umbali wa  kilomita 15  kila siku kwenda na kurudi hadi shule ya sekondari Mkako na kufika wakiwa wamechoka,lakini kwa kujengewa shule hiyo karibu itawafanya kusoma kwa bidii.

Ameiomba serikali kuwajengea mabweni ili wanafunzi hususani wa kike waweze kuishi shuleni ili wapate muda mwingi wa kusoma,badala ya kurudi nyumbani ambako wanakutana na kazi nyingi zinazowakosesha kupata muda wa kujisomea.

Hadija Mustapha amesema changamoto kubwa ni maji safi na salama,kwani licha ya kuwepo kwa mtandao wa maji lakini yanayotoka  hayafai kwa matumizi ya binadamu kwa kuwa yanatope jingi hivyo wanalazimika kutumia maji ya mvua yanatoka juu ya bati za nyumba.

Ameiomba wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini(Ruwasa)wilaya ya Mbinga,kuboresha  huduma zake ili kuwaepusha wanafunzi na walimu wa shule hiyo uwezekano wa kupata magonjwa mbalimbali ikiwamo ya matumbo na kipindupindu.

Mkuu wa shule hiyo Deniterias Mgaya amesema,katika mwaka wa masomo ulioanza tarehe 9 Januari, walipangiwa kupokea wanafunzi 184 wa kidato cha kwanza kati yao wavulana 75 na wasichana 105,na hadi kufikia wiki iliyopita wanafunzi 26 bado hawajaripoti.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.